Vurugu Bagamoyo zajeruhi,
nyumba zachomwa moto

Vurugu hizo zilianza alfajiri Agosti 15 baada ya gari aina ya Fuso
liliokuwa limebeba shehena ya marobota 189 ya nguo za mitumba na 68 ya
viatu kuacha njia na kupinduka eneo la kijiji hicho, ambapo baadhi ya
wakazi wa eneo hilo walivamia gari hilo na kudaiwa kupora mizigo na
kuihifadhi katika nyumba zao.
Baada ya tiko hilo, Polisi wa Kituo cha Chalinze
walilazimika kwenda kuongeza nguvu kutuliza ghasia hizo kutokana na
wenzao wa Kituo cha Mbwewe kuzidiwa.
Katika vurugu hizo kijana anayekadiriwa kuwa na
umri wa miaka 15 alijeruhiwa na polisi walifanikiwa kukamata watu watatu
waliohusika na tukio hilo.
Diwani wa Kata ya Mbwewe, Omar Mhando na
Mwenyekiti wa kitongoji hicho, Mashaka Kigoko walisema baada ya Fuso
hilo kuanguka, lililala katikati ya barabara na kusababisha magari
mengine yaliyokuwa yakisafiri katika barabara kuu ya Chalinze-Segera
kushindwa kuendelea na safari kwa zaidi ya saa nne, hali ambayo
iliwalazimu madereva kujikusanya pamoja ili kuwapa msaada wenzao.
“Chanzo cha huu mkasa ni hilo Fuso lililoanguka na
shehena ya mitumba na viatu, ilikatisha barabara na kuziba njia hivyo
magari mengine yalipofika hapo yalikwama, na muda ulivyozidi waliamua
kushuka na kufuatilia kulikoni na kukuta wenzao wamepata ajali,lakini
badala ya kusaidiwa kutoka garini watu walivamia na kupora mali,”
alisema Mhando.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi
amethibitisha tukio hilo na kuwa hadi saa tisa alasiri jana wanakijiji
sita ndiyo walioripotiwa kujeruhiwa.
No comments:
Post a Comment