Monday, 1 July 2013

Mapambano dhidi ya Boko Haram mipakani

Mapambano dhidi ya

 Boko Haram mipakani


Serikali ya Nigeria imetuma kikosi kikubwa cha wanajeshi pamoja na silaha kukabiliana na wapiganaji katika majimbo matatu ya Kaskazini Mashariki mwa nchi.
Taarifa kutoka kwa serikali ilisema kuwa nia ya kutumwa kwa wanajeshi hao ni kuweza kupata tena udhibiti wa sehemu ambazo inaaminika ziko chini ya udhibiti wa wapiganaji hao, pamoja na kuimarisha usalama
Mnamo Jumanne Rais Goodluck Jonathan, alitangaza hali ya hatari, katika majimbo matatu ya Yobe, Borno na Adamawa baada ya majimbo hayo kushuhudia mashambulizi mabaya sana.
Wapiganaji kutoka kundi la Boko Haram,

 wanalaumiwa kwa kufanya mashambulizi hayo.
Kundi hilo ambalo lina mizizi yake Kaskazini mwa Nigeria,limehusishwa na mauaji ya watu 2,000 tangu mwaka 2010.
Boko Haram, limedhibiti baadhi ya sehemu za kaskazini mwa nchi, kwa miaka mitatu iliyopita na nyingi ya ghasia wanazofanya zimekuwa sana sana katika eneo hilo.
Hakuna shaka kuwa hali Kaskazini mwa Nigeria inaendelea kuzorota na sasa rais Goodluck Jonathan amekiri hilo. Hakuna yeyote serikali angeweza kulitamka hilo.
Ukubwa wa mashambulizi yanayofanywa na Boko Haram, umelazimisha rais Jonathan kuchukua hatua na hata kuwanyamazisha baadhi ya wakosoaji wake wanaosema kuwa amejikokota kuchukua hatua.
Baadhi ya wadadisi wamependekeza kuwa ikiwa hali itaandelea kuzorota hivyo, itakuwa vigumu kukabiliana na kundi la Boko Haram na litaweza hata kuunda taasisi zake.
Je, wanajeshi zaidi wataweza kukabiliana na hali? kikubwa ni ambavyo wanajeshi hao wataendesha harakati zao.
Wadadisi wanasema kuwa , jeshi lina kibarua kigumu kwani kuna dalili tayari limeshindwa katika vita hivi, na raia wanahisi kuwa katikati ya mtego Nigeria

RAIS mstaafu wa Marekani, George W. Bush na mkewe


RAIS mstaafu wa Marekani, George W. Bush na mkewe, Laura wanatarajiwa kesho kuwa nchini kuhutubia kongamano linalojadili wajibu wa wake wa marais katika kuinua wanawake duniani.
bush-laura_300_172Kuwasili kwa Bush, ni mwendelezo wa wiki hii Jiji la Dar es Salaam kuwa katika pilikapilika za kupokea ugeni wa watu maarufu. Kongamano hilo limeandaliwa na Taasisi ya George Bush na litafanyika kesho na keshokutwa.
Taarifa iliyotolewa na taasisi hiyo kwa vyombo vya habari , inasema kongamano hilo litahudhuriwa na wake mbalimbali wa marais akiwemo mke wa Rais wa Marekani, Michelle Obama.
Pia Mwanzilishi wa Taasisi ya Wanawake ya Cherie, Cherie Blair atahudhuria. Wake wa marais wa Afrika watakaohudhuria ni Mama Salma Kikwete, Chantal Campaore wa Burkina Faso, Roman Tesfaye wa Ethiopia, Maria da Luz Dai Guebuza (Msumbiji), Penehupifo Pohamba (Namibia), Sia Nyama Koroma (Sierra Leone), Janet Museveni (Uganda) na Christine Kaseba wa Zambia.
Kongamano hilo litajikita zaidi katika kujadili masuala ya kuwekeza kwa wake, kuimarisha Afrika lakini pia wajibu wa wake wa marais katika kuhamasisha wanawake katika maeneo ya elimu, afya na kuwakwamua kiuchumi.

“Kongamano hili litawakutanisha pamoja wake wa marais kutoka nchi mbalimbali duniani, maofisa wa Serikali, mashirika binafsi, Asasi zisizo za Kiserikali (NGOs) na wasomi kwa ajili ya kujadili mambo muhimu ya kuchukuliwa hatua ili kuweza kuwanufaisha wanawake,” 


ilisema taarifa hiyo.
Aidha zitakazowasilishwa na kujadiliwa katika kongamano hilo ni pamoja na kuinua wajasiriamali wanawake kiuchumi kupitia mafunzo na teknolojia, kuwapatia fursa wanawake wakulima kupata mafunzo ya kilimo cha kisasa, mafunzo kuhusu saratani ya matiti na umuhimu wa elimu kwa wanawake.
Amani, utulivu na uimara wa mfumo wa demokrasia ni miongoni mwa mambo yanayotajwa kuvutia viongozi hao wa kimataifa kuja nchini.

Sunday, 30 June 2013

How the genocide happened.......in RWANDA


Some 800,000 people were killed in 
Rwanda's genocide in just 100 days

 

Rwanda:

 How the genocide happened


Between April and June 1994, an estimated 800,000 Rwandans were killed in the space of 100 days. Genocide memorial site guardian, Danielle Nyirabazungu (pictured in 2004)Most of the dead were Tutsis - and most of those who perpetrated the violence were Hutus.
Even for a country with such a turbulent history as Rwanda, the scale and speed of the slaughter left its people reeling.
The genocide was sparked by the death of the Rwandan President Juvenal Habyarimana, a Hutu, when his plane was shot down above Kigali airport on 6 April 1994.
A French judge has blamed current Rwandan President, Paul Kagame - at the time the leader of a Tutsi rebel group - and some of his close associates for carrying out the rocket attack.
Mr Kagame vehemently denies this and says it was the work of Hutu extremists, in order to provide a pretext to carry out their well-laid plans to exterminate the Tutsi community.
Whoever was responsible, within hours a campaign of violence spread from the capital throughout the country, and did not subside until three months later.
But the death of the president was by no means the only cause of Africa's largest genocide in modern times.
History of violence
Ethnic tension in Rwanda is nothing new. There have been always been disagreements between the majority Hutus and minority Tutsis, but the animosity between them has grown substantially since the colonial period.

1994: RWANDA'S GENOCIDE
6 April: President Habyarimana killed in plane explosion
April - July: Some 800,000 Tutsis and moderate Hutus killed
July: Tutsi-led rebel movement RPF captures the capital Kigali
July: Two million Hutus flee to Zaire, now DR Congo


The two ethnic groups are actually very similar - they speak the same language, inhabit the same areas and follow the same traditions.
However, Tutsis are often taller and thinner than Hutus, with some saying their origins lie in Ethiopia.
During the genocide, the bodies of Tutsis were thrown into rivers, with their killers saying they were being sent back to Ethiopia.
When the Belgian colonists arrived in 1916, they produced identity cards classifying people according to their ethnicity.
The Belgians considered the Tutsis to be superior to the Hutus. Not surprisingly, the Tutsis welcomed this idea, and for the next 20 years they enjoyed better jobs and educational opportunities than their neighbours.
Resentment among the Hutus gradually built up, culminating in a series of riots in 1959. More than 20,000 Tutsis were killed, and many more fled to the neighbouring countries of Burundi, Tanzania and Uganda.
When Belgium relinquished power and granted Rwanda independence in 1962, the Hutus took their place. Over subsequent decades, the Tutsis were portrayed as the scapegoats for every crisis.
Building up to genocide
This was still the case in the years before the genocide. The economic situation worsened and the incumbent president, Juvenal Habyarimana, began losing popularity.

President Paul Kagame (l) and his aide Rose Kabuye (r)
President Kagame (l) and his officials have denied claims they shot down the president's plane
At the same time, Tutsi refugees in Uganda - supported by some moderate Hutus - were forming the Rwandan Patriotic Front (RPF), led by Mr Kagame. Their aim was to overthrow Habyarimana and secure their right to return to their homeland. Habyarimana chose to exploit this threat as a way to bring dissident Hutus back to his side, and Tutsis inside Rwanda were accused of being RPF collaborators.
In August 1993, after several attacks and months of negotiation, a peace accord was signed between Habyarimana and the RPF, but it did little to stop the continued unrest.
When Habyarimana's plane was shot down at the beginning of April 1994, it was the final nail in the coffin.
Exactly who killed the president - and with him the president of Burundi and many chief members of staff - has not been established.
Whoever was behind the killing its effect was both instantaneous and catastrophic.
Mass murder
In Kigali, the presidential guard immediately initiated a campaign of retribution. Leaders of the political opposition were murdered, and almost immediately, the slaughter of Tutsis and moderate Hutus began.
Within hours, recruits were dispatched all over the country to carry out a wave of slaughter.
Tutsi family in a camp in 1994
Some Tutsis managed to escape to refugee camps
The early organisers included military officials, politicians and businessmen, but soon many others joined in the mayhem.
Encouraged by the presidential guard and radio propaganda, an unofficial militia group called the Interahamwe (meaning those who attack together) was mobilised. At its peak, this group was 30,000-strong.
Soldiers and police officers encouraged ordinary citizens to take part. In some cases, Hutu civilians were forced to murder their Tutsi neighbours by military personnel.
Participants were often given incentives, such as money or food, and some were even told they could appropriate the land of the Tutsis they killed.
On the ground at least, the Rwandans were largely left alone by the international community. UN troops withdrew after the murder of 10 soldiers.
The day after Habyarimana's death, the RPF renewed their assault on government forces, and numerous attempts by the UN to negotiate a ceasefire came to nothing.
Aftermath
Finally, in July, the RPF captured Kigali. The government collapsed and the RPF declared a ceasefire.
As soon as it became apparent that the RPF was victorious, an estimated two million Hutus fled to Zaire (now the Democratic Republic of Congo).
These refugees include many who have since been implicated in the massacres.
At first, a multi-ethnic government was set up, with a Hutu, Pasteur Bizimungu as president and Mr Kagame as his deputy.
But the pair later fell out and Bizimungu was jailed on charges of inciting ethnic violence, while Mr Kagame became president.
Although the killing in Rwanda was over, the presence of Hutu militias in DR Congo has led to years of conflict there, causing up to five million deaths.
Rwanda's now Tutsi-led government has twice invaded its much larger neighbour, saying it wants to wipe out the Hutu forces.
And a Congolese Tutsi rebel group remains active, refusing to lay down arms, saying otherwise its community would be at risk of genocide.
The world's largest peacekeeping force has been unable to end the fighting.

Ulinzi Mkali wa Ujio wa Obama:

Watanzania Wasikwazike 

au Kufedheheka na 

Ulinzi Mkali wa Ujio wa Obama: Ni kawaida...


Afisa wa Kitengo Maalum cha Ulinzi wa Rais akisimama helikopta ya Rais ikiondoka

Ulinzi mkali ambao tayari upo na utazidi kuonekana wakati wa Ujio wa Rais wa Marekani umewafanya baadhi ya Watanzania kujihisi wanadunishwa au kuabishwa. Wapo wengine ambao wanaona kuwa hatua mbalimbali za kiusalama zinazochukuliwa kumlinda Obama, Familia yake na ujumbe wake zinaonesha dharau na kutoaminiwa kwa vyombo vyetu vya ulinzi. Wengine wanafika mahali pa kuhisi kuwa Wamarekani wanatudharau sana kiasi kwamba wanatuchagulia nani aonene na Obama (rejea taarifa kwenye gazeti la Mwananchi la leo). Watanzania hawapaswi kujisikia hivyo hata kidogo.

Ulinzi wa Obama ni Mkali iwe ndani ya Marekani au Nje

Wakati wowote Rais wa Marekani anaposafiri iwe ndani ya Marekani au nje ya Marekani ulinzi wake ni mkali na karibu kamili (almost absolute). Kuanzia angalia ambalo anakuwepo (linakuwa no fly zone) na kuwa anaenda na kila kitu kinachoweza kutumika wakati wowote wa dharura yoyote inayoweza kufikirika kutokea. Kuanzia majanga ya moto, maji, maandamano ya kisiasa au hata mapinduzi ya kijeshi ulinzi wa Rais wa Marekani umejiandaa.

Mfano mzuri ni kuwa ikulu ya Rais pale DC – Jumba Jeupe – juu kabisa kuna mzinga wa kutungua ndege – surface to air battery. Lakini kubwa zaidi ni kuwa anga lote linalozunguka Ikulu hiyo ni eneo ambalo ndege haziruhusiwi kuruka (prohibited airspace). Na wakati wowote Rais anaposafiri mahali popote ndege haziruhusiwi kuruka juu yake. Anapotua kwenye uwanja kwa mfano hapa Detroit, hakuna ndege nyingine itakuwa inatua wakati huo huo! Sasa kama hili linatokea Marekani kwa kiasi gani linaweza kutokea Tanzania?

Ripoti hii maalum basi ina lengo la kuwasaidia Watanzania kutokwazika na kiasi cha ulinzi ambao Obama anakuja nao pamoja na usumbufu unaotokana na hilo. Kama msafara wa Rais Kikwete huwa unazusha usumbufu kwa watu basi wa Obama utasababisha kadhia – chukua msafara wa Kikwete zidisha mara 1000!

Mambo ya Kawaida ya Ulinzi wa Rais

Kwa yeye kuwa Rais wa Marekani Obama anapatiwa ulinzi wa hali ya juu kabisa labda wa kiongozi mwingine yeyote duniani. Anapokuwa ndani ya Marekani anapata bado ulinzi wa hali ya juu lakini pia ni kama mara ishirini hivi chini ya ulinzi anaopata akiwa nje ya Marekani. Hii ni kwa sababu moja kubwa anapokuwa Marekani anakuwa katika ulinzi wa vyombo vingi sana vya nyumbani na mahali popote anapokwenda. Hivyo, vitu kama magari watu, n.k vingi vinakuwa ‘mobilized’ kutoka ndani.


Ulinzi huu wa kawaida ni ule ambao mara nyingi watu wanaona (maafisa wa Usalama wanaoambatana na Obama popote anapokwenda) na ule ambao uko kwenye kivuli (usionekana) ambao unahusisha wataalamu wa mambo ya mawasiliano, wapelelezi, majasusi n.k

Rais wa Marekani anapotoka nje ya nchi anaenda pamoja na kikosi cha maaskari wasiopungua 500 hivi! Ulinzi wa Rais wetu huwa ni kama watu 40 hivi maafisa wa usalama na anapoenda nje namba hiyo inapungua kidogo. Tunaposema anakuja na watu 500 hivi kwa ajili ya ulinzi hawa ni nje ya wale wanaotangulia na wale ambao taifa husika linatoa. Kati ya hao walinzi kama 200 hivi ni makomandoo watupu wa jeshi la Marekani na Taasisi za kijasusi.
Rais Obama anaposafiri anasafiri na madaktari bingwa wasiopungua sita hivi pamoja na wapishi wake pamoja na choo chake! Pamoja na hao anaambatana na manesi na wataalamu mbalimbali wa afya ambao wanaweza kuingia kazini wakati wowote. Anapokuwa Washington DC hospitali moja iko maalum kwa ajili ya dharura ya Rais tu na ina mlango wake ambapo likitokea jambo basi Rais hatopata shida ya kuzungushwa! Pamoja na hivyo kuna kiasi cha lita za damu aina AB (damu ya Obama) ambayo pia inasafiri naye mahali popote kwa ajili ya dharura yoyote itakayohitaji kuwekewa damu. Hii ni ndani au nje ya Marekani.
Ndege ya Obama ni chombo cha ulinzi wake pia
Ndege ya Rais wa Marekani maarufu kama Air Force One siyo ndege kama ndege nyingine. Ni ndege ambayo imetengenezwa kuhakikisha kuwa Rais anapokuwa angani anakuwa salama kabisa. Imeundwa kuweza kuhimili vishindo vya mlipuko wa Nyuklia katika umbali ambao inakuwa inaruka na mabawa yake hayapigiki risasi (armor plated). Ndege hiyo pia ina uwezo wa kuingilia mawasiliano ya rada ya nchi yeyote inaporuka (radar jamming) na pia inasafiri ikiwa na makanyaboya ya mizingi ya ardhini (earth to air missiles). Ndege hiyo ina namba za simu zisizopungua 85 ambazo zinatumika wakati wote kuhakikisha kuwa Rais anaweza kuwasiliana na mtu yeyote hata anapokuwa angani.
 Obama katika ofisi yake angani
Anapokuwa ardhini helikopta za jeshi la Majini ambazo zinafuatana na rais nazo zinakuwa tayari kwa dharura yoyote. Rais wa Marekani ana helikopta 19 hivi ambazo zinaweza kutumiwa mahali popote. Hivyo, kwa mfano magari na helikopta zilizotumika Senegal si lazima zije Tanzania zinaweza kurudishwa Marekani wakati nyingine zikija Tanzania. Hili ni kweli pia kwa magari. KUtokana na ukaribu wa Afrika ya kusini na Tanzania bila ya shaka baadhi ya raslimali za ulinzi zilizotumika Afrika ya Kusini zitaletwa Tanzania vile vile.
Marine One – chopa ya Rais
Anasindikizwa na Meli za Kivita
Anapokuwa nje ya Marekani Rais wa Marekani anasindikizwa na meli za kivita zinazopokezana majukumu kwa kadiri anavyozunguka dunia na zinakuwa tayari wakati wote kuingilia kati ikibidi. Meli hizi zimejaa wanamaji na wapiganaji wa jeshi la majini (Marines). Wapiganaji wa meli hizi wako tayari wakati wowote kuingia kwenye nchi yoyote kumuokoa Rais wao endapo kuna tishio la maisha yake.
Gari lake nalo ni chombo cha ulinzi
Bila ya shaka katika ya vyombo vya ulinzi wa karibu kabisa kwa Rais ni gari lake analotumia ambalo limetengenezwa maalum kwa ajili ya kumpatia ulinzi wa hali ya juu. Hii ni pamoja na kuzuia risasi na milipuko ya mabomu ya mkono au rocket launcher! Na huwa hali moja bali kadhaa ili kuhakikisha watu hawajui Rais anakuwa katika gari gani hasa.


Limo – full armored

Rais anapokuwa ndani ya nchi nyingine
Rais wa Marekani anapokuwa ndani ya nchi nyingine suala la usalama linakuwa kwa kiasi kikubwa mikononi mwa nchi husika – kiufundi tu. Kimsingi hata hivyo ulinzi wake unahakikishiwa na Marekani na vyombo vyake vya ulinzi. Nchi husika na vyombo vyake vya ulinzi vinakuwa na mawasiliano ya mipango na hawa Wamarekani. Kutegemeana na nchi nan chi baadhi ya nchi zinaruhusiwa kwa kiasi kikubwa na nchi nyingine zinaona ni bora kuwaachia Wamarekani waendeshe ulinzi wenyewe – ili kukwepa lawama. Hivyo, Obama akienda Israeli kwa mfano walinzi wa Kiisraeli wanapewa nafasi kubwa kuliko kwa mfano akienda Afghanistan!



Lakini popote anapokwenda nchi husika inakuwa nyuma ya Wamarekani katika masuala ya ulinzi. Hili ni muhimu kulizingatia hasa kwa wale ambao wanaweza kudhani kuwa kwa kusisitiza kuwa Wamarekani wasimamie ulinzi wa Obama akiwa Tanzania basi Wamarekani wametudharau. Hili si kweli. Wamarekani wanatoa ulinzi huu wakishirikiana na watu wetu lakini kutokana na uzito wa ujumbe wenyewe na hasa hali ya usalama katika eneo letu (ikumbukwe tayari kulishatokea milipuko dhidi ya Wamarekani na wapo wenye kuvionea huruma vikundi vya kighaidi) ni wazi kuwa Wamarekani watakuwa na sharti la kusimamia ulinzi wote wao wenyewe na hilo sisi wengine tushukuru tu na labda kujifunza.



Japo wengi watauona ule ulinzi ulioko kwenye msafara ambao kwa kweli ni kidogo tu – ulinzi wenyewe ni ule ambao uko nje ya msafara; watakuwa kwenye mapaa, kwenye mahoteli, kwenye barabara na wengine watakuwa katikati ya watu wamechanganyika. Fikiria kwa mfano alipoenda India kiasi cha ulinzi kilikuwa karibu maafisa 10,000 wakitengeneza kama ngazi tano za ulinzi – na ninaamini hili litatokea Tanzania pia. Kulikuwa na watu karibu 1000 kwenye ziara ya India ambao walikuwa wanamlinda Obama ambao ni Wamarekani watupu!

Baadhi ya maafisa wanaomlinda Obama wanavaa miwani zenye camera ambazo zinarekodi na kurusha moja kwa moja sura na watu mbalimbali anaokutana nao au wanaojitokeza kumpokea. Yote ni katika kuhakikisha usalama

Kwenye njia zote ambao Obama na mke wake watakuwepo kutakuwepo na walenga shabaha (snipers) na majasusi wakitoa ulinzi. Kama Obama atalala Ikulu basi kutakuwa na maofisa wa Kimarekani wasiopungua 2000 hivi kuongeza ulinzi wa Ikulu yetu na kufanya Ikulu hiyo kuwa jengo salama zaidi duniani kwa usiku huo! Hili litakuwa pia kweli kama atalala kwenye mojawapo ya mahoteli yetu makubwa Jijini Dar. Kwenye nchi nyingine ambazo Rais hawezi kulala kwenye nchi husika basi meli ya kijeshi ya Kimarekani iliyoko karibu inageuzwa kuwa hoteli na wakati mwingine atalala angani wakati anarejea kwao!

Njia zote zina mbadala wake

Njia zote ambazo Obama atapitia tayari zitakuwa na mbadala waka (alternative routes) kiasi kwamba jambo moja likitokea kwenye njia moja tayari wanajua ni njia gani nyingine wachukue. Ni kwa sababu hiyo labda watu wa Dar-es-Salaam wameshauriwa kuangalia kama wanasababu ya kwenda mjini. Usumbufu wa aina hiyo hautatokea Dar tu na watu wakakwazika hata anapokuwa hapa usumbufu huo wengine tunaupata.


Mara mbili nimewahi kujikuta katikati ya mahali ambapo Rais anasafiri au kuja. Mara ya kwanza ilikuwa mara baada ya tukio la Septamba 11 wiki chache baadaye Rais Bush alikuja Detroit na alikuwa na mkutano hoteli moja iliyokuwa upande wa pili wa hoteli ambayo nilikuwa nafanyia kazi. Wakati huo nikifanya kazi kwenye mambo ya corporate reservations. Wiki kadhaa nyuma maajenti wa SS walikuja na kubook sakafu nzima ambayo haturukuhusiwa kumweka mtu yeyote!

Mara ya pili mwaka jana wakati wa kampeni katika misafara yangu nikajikuta nabadilishiwa njia mahali ambapo palikuwa pamejaa mapolisi na barabara imefungwa – kisa Obama alikuwa na chakula cha jioni nyumbani kwa mtu mmoja wa wafadhili wake!

Hivyo, Watanzania wanapopata ugeni huu wasikwazike sana kama mawasiliano yao yataingiliwa – hasa wanaoishi Dar kwa sababu ya kuhakikisha kuwa hakuna bomu linaloweza kulipuliwa kwa simu – na hata kupata usumbufu mkubwa. Obama anakuja akiwakilisha taifa lenye nguvu kubwa zaidi duniani; nguvu hii kwa kiasi tu Watanzania wataiona na itawasumbua. Kwa wale wanaofikiria labda Obama ni kama Rais wa China wafikirie tena; ulinzi wa Obama ni mara nyingi zaidi ya ulinzi wa Xi Jinping.

Kwa hiyo kama ulishaanza kukwazika na kuona umedharauliwa hauna sababu tena; shangaa, furahia, jifunze na ombea aje na kuondoka salama yeye na msafara wake wote. Wakishaondoka, pumua kwa furaha.

Waandishi wa Tanzania na Watanzania wasiogope kuwapiga picha aafisa wa usalama wakiwa kazini. Hakikisha tu kwamba ukifanya hivyo huwawekei kizuizi wakiwa kazini.

Wafanyabiashara changamkia..Biashara na USA



Wafanyabiashara changamkia

 ujio wa Obama



Rais Barack Obama anawasili nchini kesho kwa ziara ya siku mbili. Pamoja na kufuatana na familia yake, Rais huyo pia ataongoza ujumbe wa watu zaidi ya 700 wengi wao wakiwa wafanyabiashara wakubwa wanaotafuta fursa za uwekezaji hapa nchini.
Hivyo, asijidanganye mtu kwamba Rais Obama na ujumbe wake wa wafanyabiashara wanakuja nchini kupiga siasa au kuimbiwa ngonjera na taarabu. Wala asijidanganye mtu kwamba Marekani imefanya madhumuni ya ziara hiyo kama siri kubwa ili nchi hiyo iweze kuwazuga na kuwahadaa viongozi wetu kwa lengo la kuchukua rasilimali zetu kirahisi.
Marekani tayari imeitangazia dunia na wananchi wa Marekani waliokuwa wakiikosoa ziara hiyo wakidai ingekuwa mzigo kwa walipa kodi wa nchi hiyo, kwamba ziara hiyo ni muhimu kwa uchumi wa Marekani na kwamba nchi hiyo ilifanya makosa makubwa kuiachia China kujitanua na kujiimarisha barani Afrika kwa kuingia mikataba ya kiuchumi na nchi mbalimbali. Ziara ya Rais Xi Jinping wa China nchini Tanzania hivi karibuni pia imeizindua Marekani kutoka usingizini, hivyo kaulimbiu ya Marekani hivi sasa ni ‘kutangulia sio kufika’.
Watanzania tunapaswa kuuona ujio wa Rais Obama na ujumbe wake katika muktadha huo. Ni ujio wa kibiashara na kiuchumi ambao Serikali na wafanyabiashara wetu wakijipanga vizuri na kutanguliza weledi na uzalendo nchi yetu nayo itafaidika na ziara hiyo. Katika mazungumzo na mapatano na ujumbe huo kabla ya kusaini mikataba, mkakati wetu kitaifa uwe ‘nipe nikupe’ na tusikubali hata kidogo kuingia tena mikataba ya ghiliba na ya ujanjaujanja.
Jambo muhimu hivi sasa ni kuwauliza wafanyabiashara na viongozi wa Serikali jinsi walivyojipanga kuingia katika mazungumzo na ujumbe huo. Tusijidanganye. Ujumbe wa Rais Obama utakuwa na wataalamu wa hali ya juu wa mapatano ya kibiashara za kimataifa (international trade negotiators).
Kwa kawaida, wengi wao huwa ni maprofesa waliobobea wa vyuo vikuu ambao wana nadharia na ujuzi mkubwa katika kile kinachoitwa mchezo wa mapatano (negotiation game). Hivyo, Wamarekani wataingia kwenye mapatano wakiwa tayari wanajua watoe nini na wachukue nini, kwa maana ya kutawala mchakato mzima na kujua ni wakati gani wasonge mbele au warudi nyuma.
Ni wazi kwamba itakuwa balaa kubwa kwa nchi yetu iwapo wawakilishi wetu wataingia katika mazungumzo hayo kichwakichwa. Tatizo tunaloliona hapa ni kwamba mazungumzo hayo yatahusu pia masuala yanayohitaji utaalamu wa hali ya juu, yakiwamo uchimbaji wa gesi, mafuta, urani na madini. Sisi hatuna wataalamu wazalendo waliobobea katika nyanja hizo, hivyo tunaishauri Serikali isione haya kutafuta washauri mabingwa waelekezi ambao ni waaminifu na waadilifu ili washiriki katika mazungumzo hayo.
Huu sasa ni wakati mwafaka kwa nchi yetu kutumia ushindani wa kibiashara kati ya Marekani na China ili tunufaike. Serikali ijipange vizuri kuweka wazi sera za nchi kuhusu biashara ya nje na matumizi ya rasilimali zetu na itayarishe maeneo ambayo tayari imetenga kwa wawekezaji.
Ni matarajio yetu kwamba wafanyabiashara wetu katika sekta binafsi katika nyanja za utalii, biashara na viwanda nao watajipanga vyema kukutana na wenzao kutoka Marekani. Jambo wanalopaswa kuzingatia ni kwamba ujumbe wa Rais Obama unakuja nchini kutafuta fursa za kibiashara na kiuchumi na siyo vinginevyo.

LOWASSA AMTAKA OBAMA ....


Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo yaNje na Ushirikiano wa Kimataifa, Edward Lowassa, amemtahadhalisha kujiepusha na kauli za kuunga mkono ushoga.
 

Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, ameliambia NIPASHE Jumapili ofisini kwake jijini hapa jana kuwa ushoga na hai za ndoa kwa watu wa jinsia moja vinaweza `kuiharibu’ ziara yake hapa nchini.

Mapema wiki hii, Rais Obama alikaririwa akizungumzia masuala hayo yanayotajwa kuwa ni moja ya haki za msingi za binadamu, alipokuwa Senegal, lakini akapingwa.
 

“Watanzania hawatalikubali na wataendelea kushikilia uhuru na heshima walizojengewa tangu awali, kwamba ushoga na ndoa za jinsia moja havikubaliki,” alisema.

Akiwa Senegal, Rais Obama alitaka serikali za Afrika kutoa haki kwa mashoga kama inavyotoa kwa raia wengine.
 

"Ninachotegemea, I pray and hope (ninasali na kutegemea) kwamba kuhusu mashoga na ndoa za jinsia moja, Rais Obama hatarudia kauli aliyoitoa kule Senegal,” alisema.

Aliongeza, "ninasema hivi kwa sababu Tanzania hatuamini katika ushoga, na endapo utawalazimisha Watanzania, watakukatalia na kushikilia uhuru na heshima waliyojengewa toka awali."

AHIMIZA MAPOKEZI MAZURI
Rais JK & Lowasa

Hata hivyo, Lowassa aliwataka Watanzania kuiheshimu na kuitumiavema fursa ya kutembelewa na Rais Obama, hivyo wajitokeze kumlaki kwa wingi.
 

"Tutambue mataifa makubwa yanakimbilia maslahi ya karne inayofuata, kwa mfano Rais wa China, Xi Jiping siku moja baada ya kuapishwa kwake alikuja hapa nchini, " alisema.
 

Hivyo, alitoa wito kwa Watanzania kuhakikisha maslahi na fursa za kiuchumi zinakuwa za kwanza kulindwa, kwa kuwa ziara hiyo itafungua milango zaidi kwa wawekezaji kuja nchini.
 

Pia, Lowassa alisema ziara ya Rais Obama ni kielelezo cha amani na usalama uliopo, na kwamba itasaidia kuwavutia watalii na wadau wa sekta nyingine za maendeleo kuitembelea Tanzania.

KITUO CHA KIJESHI
Kuhusu hofu na tetesi kuwa ziara hiyo imelenga taifa hilo kuja hapa nchini kufungua kituo cha kujiimarisha kiulinzi, Lowassa alisema Watanzania wanapaswa kufahamu kuwa tayari nchi hiyo ina kituo cha kijeshi nchini Kenya.


"Tuangalie maslahi yetu tuachane na mitazamo hasi, kama ni kituo cha kijeshi tayari kipo Kenya, tujiulize kwa nini marais wa Marekani Bill Clinton na George Bush walivyofanyaziara zao hapa nchini hawakwenda Kenya," alisema.

WALINZI WA NDANI KUWEKWA KANDO
Kuhusu ziara hiyo kutumia ulinzi wa kimataifa huku majeshi ya Tanzania yakiwekwa kando kwa ushiriki wa moja kwa moja, Lowassa alisema Rais wa Marekani ana kiwango cha juu cha ulinzi unaosimamiwa na nchiyake pekee.
 

"Ni sahihi walinzi wetu kukaa pembeni, huyu ni kama Rais wa dunia, lakini hata majeshi yetu yanafanya kazi ya ulinzi lakini sio kwamba yatakaa nyuma tu," alisema.
 

SUMAYE: TUMKARIBISHE
Naye, Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, alisema ziara ya Rais Obama haina ujumbe zaidi ya kuhimiza watu wajitokeze kumpokea.
 

Hata hivyo, Sumaye alikwepa kuzungumzia kwa undani hatua ya kuwafukuza wafanyabiashara kutoka kandoni mwa barabara, ili kupisha mapokezi ya Rais Obama.
 

“Ninachokielewa ni kuwa barabara ambazo wanapita viongozi kama Rais Obama zinatakiwa kuwa katikahali ya usalama na hivyo kutakiwa kuboreshwa,” alisema.

LIPUMBA: MAFANIKIO NI MADOGO KIUCHUMI
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, alisema mafanikio ya ziaraya Rais Obama yapo katika kujitangaza kimataifa kuliko kiuchumi.
 

Profesa Lipumba ambaye ni mchumi aliyebobea, alisema changamoto iliyopo ni kwamba bado biashara kati ya nchi mbili hizo siyo kubwa kama ilivyo kwa nchi kama China na Tanzania.
 

Alitolea mfano, mwaka 2012 bidhaa za hapa nchini zilizouzwa Marekani zilikuwa na thamani ya Dola milioni 66 ikilinganishwa na zile zilizouzwa China ambapo zilikuwa ni zaidi ya Dola milioni 500.
 

Alisema bidhaa zilizoagizwa kutoka Marekani zilikuwa na thamani ya Dola milioni 230 huku za kutoka China zikiwa na thamani ya zaidi ya Dola milioni 1,100.

"Utakubaliana nami kuwa mahusiano yetu na China ni makubwa kuliko Marekani licha ya nchi hii kutoa fursa kwetu ambazo hatujazitumia ipasavyo," alisema
 

Profesa Lipumba alisema Marekani kupitia mpango wake wa kusaidia Maendeleo ya Afrika (AGOA), ulitoa fursa kwa bidhaa za Afrika kuuzwa nchini humo bila ushuru, lakini Tanzania haikuitumia.

Pia alisema utawala wa George Bush, uliisaidia Tanzania kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millenium Challenge Compact (MCC) kupewa Dola milioni 700 kwa ajili ya kusaidia miundombinu na ujenzi wa nyaya za umeme kutoka bandarini hadi Zanzibar.

"Pana uwezekano wa mpango wa pili wa MCC, Tanzania ikapata msaada wa kuimarisha miundombinu ya umeme, lakini pia kampuni za Marekani kuja kuwekeza hapa kwetu," alisema.
 

Alisema uwekezaji wa kampuni hizoutategemeana na wafanyabiashara wa hapa nchini pamoja na serikali kutumia fursa mbalimbali za nchi hiyo.
 

Katika hatua nyingine, Profesa Lipumba alisema ili nchi iweze kujikwamua na umasikini itatokana na jinsi itakavyotumia sera na juhudina siyo kutegemea msaada kutoka nje.
 

HOTELI ZIMEJAA
Wingi wa wageni wakiwamo watakaofika kwa ajili ya ziara ya Rais Obama, umesababisha hoteli nyingi za jijini Dar es Salaam `kujaa’.
 

Uchunguzi wa NIPASHE Jumapili ulibaini kwamba kwa zaidi ya wiki sasa, hoteli nyingi hazikupokea wageni kutokana na kile kilichoelezwa kuwa, nyingine zililipiwa ingawa vyumba havikutumika kwa wakati.
 

POLISI: WASIO NA KAZI WASIJE MJINI
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga, amewataka wananchi ambao hawatakuwa na mambo muhimu ya kufanya katikati ya jiji, wasifike huko kupunguza msongamano wa watu na magari baada ya kuwasili kwa Rais Obama.
 

Alisema, baadhi ya barabara zitafungwa kwa muda kwa ajili ya viongozi kuzitumia, hivyo kusababisha msongamano.
 

Hekaheka zimetanda jijini Dar es Salaam, ikiwa ni zaidi ya saa 24 kabla ya kuwasili kwa Rais Barack Obama.
 

Rais Obama, atawasili nchini kesho akitokea Afrika Kusini, ambapo pamoja na mambo mengine, alizungumza katika mkutano wa ‘viongozi vijana wa Afrika’ na kujibu maswali kutoka nchi tofauti.
 

Mkutano huo ulifanyika jana jioni huko Soweto nchini Afrika Kusini, ambapo alipokewaa na kujibu maswali kutoka Kenya, Uganda, Nigeria na Afrika Kusini kwenyewe.
 

Jijini Dar es Salaam, shughuli kadhaazikiwamo za ulinzi na usalama, zinafanyika kwa kasi na umakini kuhakikisha ziara ya Rais Obama inafanyika pasipo bughudha. kujibu maswali kutoka Kenya, Uganda, Nigeria na Afrika Kusini kwenyewe.
 

Jijini Dar es Salaam, shughuli kadhaazikiwamo za ulinzi na usalama, zinafanyika kwa kasi na umakini kuhakikisha ziara ya Rais Obama inafanyika pasipo bughudha.
 

Hata hivyo, sehemu kubwa inayohusu masuala ya itifaki, ulinzi na usalama yanafanywa na taasisi za Marekani, kwa kuzishirikisha taasisi za ndani kwa kiwango kidogo.
 

“Hawa jamaa (Wamarekani) wanapoingia nchi yeyote wakiwa naRais wao, shughuli nyingi na uamuzi wanafanya wao, sisi wa ndani inakuwa kushirikishwa kwa kiasi kidogo,” kilieleza chanzo cha NIPASHE Jumapili kutoka moja ya taasisi zinahusika katika ziara hiyo.
 

Maeneo kadhaa ya jijini humo, yaliendelea kudhibitiwa kwa ulinzi mkali na doria za mara kwa mara, huku kandoni mwa baadhi ya barabara wakionekana askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ).
 

Mathalani, kandoni mwa barabara ya Morogoro, eneo la Ubungo, walionekana askari wa JWTZ maarufu kama MP.
 

Shughuli nyingine zimehusisha pia operesheni zinazofanywa na polisi kwa kusaidiana na mgambo wa jiji, kuhakikisha watu na bidhaa zilizopokandoni mwa barabara zitakazotumika kwa ziara ya Rais Obama, vinaondolewa.
 

Magari yaliyowabeba polisi wenye silaha za moto na mabomu ya machozi, yalionekana katika mitaa kadhaa jijini humu, wakihakikisha operesheni hiyo inafanyika pasipo kikwazo kutoka kwa wahusika.
 

Kila palipofanyika operesheni hiyo, baadhi ya askari walifanya doria zamu kwa zamu, kuhakikisha kuwa bidhaa na watu walioondolewa, hawarejei.
 

Hata hivyo, waathirika katika operesheni hiyo walieleza kutofurahia, huku wakihoji ni kwa nini serikali haikuwaandalia mazingira mbadala kabla ya utekelezaji wake. 
 
Walisema miongoni mwao, wamekopa mitaji kutoka kwenye taasisi za kifedha, hivyo kusimamisha biashara zao ili kupisha ujio wa Rais Obama, kutawaweka katika hali ngumu kiuchumi.
 

“Ikiwa ujio wa Rais Obama unatutesa wafanyabiashara kiasi hiki, ni vigumu kuhimili maisha yetu, kwa sababu hatujui hatma yetu baada ya yeye kuondoka,” alisema mfanyabiashara Zena Rashidi wa Kariakoo.
 

Hata hivyo, wamachinga walionekana jana katika kituo cha mabasi cha Mwenge walipofukuzwa, wakiwa wanaendelea na biashara zao.

Lakini walifanya hivyo kwa tahadhali ikiwamo kushika bidhaa chache mikononi, huku wakitumia 'janja' ya kupiga kelele za 'kumsifia' Rais Obama.
 

Walisikika miongoni mwao wakisema, 'praise to Obama' na wengine wakaitikia 'aaamen'. Walifanya hivyo zamu kwa zamu, lakini haikujulisha waliashiria nini.
 


BARABARA ZAPAMBWA
Aidha, barabara zote atakazopita Obama wakati wa ziara yake zimepambwa kwa bendera za Marekani na Tanzania; huku zikinakshiwa kwa picha yake ambayo imeandikwa 'President Barack Obama' karibu Tanzania.
 

Barabara hizo ni ile ya Nyerere kuanzia uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Mwai Kibaki na Bagamoyo.

NIPASHE Jumapili imeshuhudia pichana bendera hizo zikiwa zimewekwa kwenye mabango yote yaliyo barabarani kuanzia Ikulu hadi kwenye barabara hizo huku usafi wa jiji ukionekana kuimarika zaidi.
 

Jana gazeti hili lilishuhudia karibu barabara zote, vijana wanaofanyakazi ya kuweka bendera na picha ya Obama wakifanyakazi hiyo.

Saturday, 22 June 2013

Alichokisema bungeni

Nchemba, Msigwa nusura 

wazichape Dodoma


msigwa
Dodoma. Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa na mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba jana nusura wachapane makonde baada ya kutupiana maneno ya kashfa, wakituhumiana kuhusika na mlipuko wa bomu uliotokea Jumamosi iliyopita mkoani Arusha.
Tukio hilo lilitokea katika viwanja vya Hoteli ya St Gasper nje kidogo ya mji wa Dodoma, walipokwenda kwa ajili ya kuhudhuria semina ya wabunge wapambanaji na Ukimwi, ambapo baadhi ya wabunge wa Chadema walihudhuria, baada ya kutoonekana mjini humo tangu Juni 17 mwaka huu.
Wabunge hao wa Chadema hawakuhudhuria kikao chochote cha Bunge kutokana na kwenda mkoani Arusha kwa shughuli mbalimbali, kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea katika mkutano wao wa kuhitimisha kampeni zake za uchaguzi mdogo wa udiwani katika viwanja vya Soweto, Juni 16 jijini humo.
Malumbano hayo yanatokana na Nchemba kuituhumu Chadema kuhusika na mlipuko huo, Juni 20 mwaka huu wakati akichangia hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2013/2014, akisema chama hicho kilipanga kulipua bomu hilo ili kuwafanya Watanzania waamini kuwa Serikali ya CCM ndiyo inayohusika na tukio hilo.
Ilivyotokea
Wakati Msigwa akiingia katika ukumbi huo akiwa ameongozana na Mbunge wa Nyamagana (Chadema), Ezekiah Wenje, walikutana uso kwa uso na Nchemba ambaye alikuwa akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Said Amour Arfi.
Baada ya Nchemba kumwona Msigwa alimkaribisha mchungaji huyo akisema; “Karibu sana bwana, salama lakini?”
Hata hivyo, badala ya kujibu salamu hiyo ya Nchemba, Msigwa alikuja juu na kumtuhumu Nchemba kwamba anatoa kauli zinazoweza kuvuruga amani ya nchi.
“Wewe ni mtu hatari sana, haya yote yanasababishwa na wewe, mnatumia damu za watu kutafuta madaraka,” alisema Msigwa akimtupia maneno Mwigulu.
Baada ya kauli hiyo Nchemba alihoji akisema: “Ki-vipi? Hayo mambo tuyaache, Msigwa achana na haya mambo!”
Baada ya Nchemba ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM kujibu, Msigwa alimsogelea karibu na kumnyooshea kidole, huku akiendelea kumtuhumu kuwa ana siasa chafu zinazopandikiza chuki kwa jamii.
Malumbano hayo pia yaliingiliwa na Mbunge wa Musoma Mjini (Chadema), Vicent Nyerere ambaye alimuunga mkono Msigwa, huku akimtuhumu Nchemba kuwa ni mtu mbaya katika siasa za Tanzania. Katika kile kilichoonekana kutaka kuweka mambo sawa, Wenje alimvuta Msigwa na kumpeleka ukumbini ili kuepusha shari baada ya wabunge hao kuzidi kurushiana maneno.
Hata walipoingia ndani ya ukumbi huo wabunge hao waliendelea kulumbana, lakini wakatulizwa na baadhi ya wabunge waliokuwa karibu yao.
Alipotakiwa kueleza sababu za mzozo huo na Nchemba, Mchungaji Msigwa alisema, “Achana na yule mpuuzi, mimi siwezi kuzungumza na mtu mnafiki, mkatili na yeye ndiye alihusika na mipango mibaya dhidi ya Chadema hata mlipuko wa Arusha hivyo kutesa watu wa Chadema.”
Alisema kuwa yeye haoni sababu ya mtu mwenye mipango mibaya na wananchi wa Tanzania pamoja na chama chake (Chadema), kuwafuata na kujikomba.
Kwa upande wake Nchemba alipoulizwa alisema kuwa alichokizungumza ni mtazamo wake na kwamba ikiwa kuna mtu anayeona kuwa alizungumza uzushi, ajitokeze na kupinga. “Nilichokizungumza ndicho kilichofanyika kwa matukio yote niliyoeleza bungeni,”alisisitiza Nchemba.
Alichokisema bungeni

Wakati akichangia mjadala wa Bajeti, Nchemba alisema hata ripoti iliyotolewa na Jukwaa la Wahariri baada ya kutekwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Absalom Kibanda, ilieleza kuwa watu waliohojiwa walidai kuwa Chadema kimepewa mafunzo kutoka nje ya nchi, kwamba kikitumia baadhi ya viongozi wa dola wasiokuwa waaminifu kuteka watu na hata kuua watu maarufu, watu wataamini CCM imeshindwa kuongoza nchi na sasa imeanza kuua watu.

Akizungumzia mkanda wa video unaoonyesha tukio la mlipuko wa bomu la Arusha, Nchemba alisema kuwa tukio hilo lilipangwa na ndiyo maana Chadema walipanga hadi wakarekodi tukio hilo.
“Lile tukio limepangwa na ndiyo maana hata aliyechukua ile video hakustushwa kabisa na mlipuko wa bomu, jambo hilo haliwezekani kabisa, tukio lile limepangwa kwa kiwango cha chini kabisa,” alisema na kuongeza; “Mtu yule alikuwa akichukua video utadhani yuko katika harusi,
CCM haijashiriki katika tukio la Arusha, ila kutokana na nguvu ya chama hiki ni lazima kitahusishwa na tukio hilo.”