Thursday 22 August 2013

MKAPA NA MWINYI WAWASILI LIVE ZIMBABWE

 

 
Tanzania

 

MKAPA NA MWINYI WAWASILI LIVE 

ZIMBABWE KUHUDHURIA KUAPISHWA 

JONGWE

 

KWA MUGABE AT AGE 89!!




Marais Wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa na wake zao, Mama Sitti Mwinyi na Mama Anna Mkapa, wakiondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kuelekea Harare, Zimbabwe, kushiriki katika sherehe ya kuapishwa kwa Rais wa Zimbambwe, Mhe Robert Mugabe, inayotarajiwa kufanyika kesho Alhamisi Agosti 22, 2013


Marais Wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa na wake zao, Mama Sitti Mwinyi na Mama Anna Mkapa, wakiwasili katioka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Harare, Zimbabwe, walikoalikwa kushiriki katika sherehe ya kuapishwa kwa Rais wa Zimbambwe, Mhe Robert Mugabe, inayotarajiwa kufanyika kesho Alhamisi Agosti 22, 2013.PICHA NA IKULU
Karibu Tanzania
 


Fisi mawindoni....

 
 
Fisi Mawindoni
MANISPAA ILALA YASIMAMISHA WATENDAJI 
WAKE KWA UBADHIRIFU
Ubadhilifu Halimashauri

Baraza la Madiwani la Manispaa ya Ilala limewasimamisha kazi watumishi wanne wa Manispaa hiyo kwa vitendo mbalimbali vya ubadhirifu wa mali za umma pamoja na uwajibikaji usioridhisha.
Hatua hii imekuja baada ya Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kukataa kupokea taarifa za mapato na matumizi za Halmashauri ya Ilala baada ya kubaibni ubadhirifu wa zaidi ya shilingi bilioni 2/=. Aidha Baraza la Madiwani limeagiza watumishi wengine 21 kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

Maamuzi hayo yalitangazwa na Meya wa Manispaa hiyo, Ndugu Jerry Silaa, ambaye aliwataja waliosimamishwa kuwa ni mhandisi wa Manispaa ambaye anatuhumiwa kwa kusimamia ujenzi na sheria za mipango miji. Tuhuma nyingine za Mhandisi huyo ni pamoja na kushindwa kusimamia ukarabati wa barabara mjini na matumizi yaayotia mashaka ya fedha za ukarabati wa barabara, kutoa kibali cha ujenzi wa ghorofa 14 katika mtaa wa Indira Gandhi wakati kwa mujibu wa sheria zilizopo eneo hilo inaruhusiwa kujenga majengo yasiyozidi ghorofa 10.

Mtumishi mwingine aliyesimamishwa ni Mkuu wa kitengo cha ukaguzi wa majengo kwa kushindwa kusimamia ujenzi wa majengo kwa mujibu wa sheria zilizopo. Aidha, anatuhumiwa kuchangia ajali ya jingo lililoanguka katika mtaa wa Indira Gandhi na kusababisha vifo vya watu 36 na wengine kujeruhiwa.
Aidha katika watumishi ambao Baraza la Madiwani limeagiza kuwa wachukuliwe hatua za kinidhamu ni pamoja na KAimu Ofisa elimu Sekondari na Kaimu Ofisa Elimu Msingi katika manispaa hiyo.
 
KETU TANGA
 

Tuesday 20 August 2013

JWTZ kushiriki mazoezi Angola

Simba wa Tanzania

JWTZ kushiriki mazoezi 

Angola




JWTZ...
Dar es Salaam. Maofisa na Askari 35 wa Jeshi la
Wananchi (JWTZ), kutoka Kamandi ya Jeshi la Anga wameondoka nchini jana kuelekea Angola kushiriki mazoezi ya kijeshi ya Blue Zambezi ambayo yanatarajiwa kuanza nchini humo leo (Agosti 20) hadi Agosti 31 mwaka huu.
Akizungumza wakati wa kuwaaga maofisa hao katika Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam jana, Meja Jenerali Hassan Vuai Chema aliwataka wanajeshi hao kuonyesha nidhamu ili kujenga ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na nchi zingine za Jumuia ya Mandeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
JWTZ

“Mkiwa Angola mna jukumu la kufanya kazi kwa bidii, kujifunza na kutoa kwa wengine kile ambacho tunacho ili wengine wajifunze kutoka JWTZ” 

alisema Meja Jenerali Chema na kuongeza kuwa katika msafara huo kuna maafisa 21 na askari wa kawaida 14.
Alisema kuwa msafara huo utaongozwa na Brigedia Jenerali Azra Ndimgwango na mazoezi hayo yanashirikisha vikosi vya jeshi kutoka nchi zingine za SADC yakiwa na lengo la kuwaandaa wapiganaji hao kutoa msaada mara nchi moja inapotokewa na majanga.

“Tunawandaa wawe tayari yanapotokea majanga kama vile usambazaji wa chakula, dawa na vifaa vingine”

alisema na kuongeza kuwa mafunzo hayo ambayo yatahusiaha matumizi ya helikopta katika kukabiliana na majanga anaamini yatapanua zaidi upeo wa wanajeshi wa nchini katika kukabiliana na majanga.

kwetu Tanga