Wednesday 11 September 2013

SADC : KAGAME UKIISHAMBULIA TANZANIA, TUTAKUPIGA


 
 
 
 
Taarifa
 
Rwanda
SADC
 
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imetoa onyo kali kwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kwa kumtaka aachane mara moja na na fikra zozote mbaya alizonazo ikiwamo mipango yake ya kuihujuma Serikali ya Tanzania na watu wake.

Onyo hili limefuatia nchi wanachama wa SADC kufuatilia kwa makini mzozo wa kidiplomasia ambao Kagame aeuiubua na amekuwa anaukuza hadharani na kichinichini dhidi ya Rais Jakaya Kikwete na Tanzania kwa ujumla.

Habari hizi zimetolewa na viongozi wa juu wa SADC na maofisa wa Serikali, waliokuwa katika ujumbe wa Rais Jakaya Kikwete alipokwenda kuhudhuria Mkutano wa viongozi wa Maziwa Makuu huko Uganda hivi karibuni. Aidha, imethibitishwa kuwa tayari Jumuiya hiyo imekwisha mpatia ujumbe huo mmoja wa mawaziri aliyekuwa ameandamana na Kagame muda mfupi baada ya kikao chake na Kikwete.

Kiongozi mmoja wa juu wa Msumbiji ambaye alikuwa pia Uganda, alikaririwa akimueleza Waziri aliyeandamana na Kagame kuwa “Nchi za SADC zinafahamu kuwa Rais Kagame hajafurahishwa na uamuzi wa Tanzania wa kupeleka vikosi vyake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC. Hata hivyo Kagame anapaswa kuelewa kuwa ilichofanya Tanzania ulikuwa ni msimamo wa pamoja wa nchi za SADC."

Aidha Kiongozi huyo aliendelea kusema "hivyo basi vitisho au uvamizi wa kijeshi dhidi ya Tanzania utachukuliwa ni uvamizi dhidi ya SADC, na tutakuwa tayari kuingia vitani kupigana upande wa Tanzania.”
 
 

Sunday 8 September 2013

KOMSALA WILAYANI HANDENI....Yatoa somo.

 
 
 
Sharobaro
 
MSHAMBULIAJI hatari wa timu ya Mashorobaro iliyopo kijiji cha Komsala, wilayani Handeni, mkoani Tanga, Malilo Gerevas, amesema kwamba wataendelea kuwanyanyasa watani wao wa jadi, Men Stone kwa kuwafunga kila wanapokutana uwanjani.
Timu zote mbili zinapatikana katika kijiji hicho kinachotajwa kuwa na msisimko wa aina yake katika mpira wa miguu kiasi cha kuleta raha kwa wadau wa michezo     maeneo hayo.
Akizungumza na Handeni Kwetu Blog kijijini kwao juzi, Gerevas alisema kwamba wao wana timu nzuri na iliyosheheni vijana wadogo, jambo linalowafanya wawe na kasi uwanjani.
“Wale ni ndugu zetu lakini katika masuala ya soka wataendelea kulia kila siku kwakuwa lazima tuwafunge ili waone namna gani sisi ni bora kuliko wao tunapokuwa dimbani".
“Sisi wote zamani tulikuwa timu moja ya Men Stone, ila tukaona hamu ya kuanzisha timu nyingine na kuitwa Masharobaro na kufanikiwa kuonyesha shauku yetu michezoni,” 
 
 alisema Gerevas.
Licha ya kuwa na shauku kubwa ya kuendeleza vipaji vyao, ila Gerevas ni miongoni mwa vijana wengi wanaoshindwa kuonyesha cheche zao kutokana na ukosefu wa mipango ya kukuza soka la vijana katika wilaya ya Handeni, mkoani Tanga.
 
Kwetu Tanga