Saturday 1 June 2013

UTAJIRI WA MKOA WA KAGERA

MAMA TERESIA
 Kipepeo wapatikanao minziro na ni hazina ya utali katika poli la minziro katika msimu huu vipepeo wamekuwa wengi huku kwetu minziro karibu ujionee majina ya vipepeo ni ya kubuni tukizingatia mtu aliye mkamata na kutiletea ....na kumuweka rangi nyekundu kanma alama na kutaka kujua anauwezo wa kusafiri umbari gani........mama teresia alikutwa amefariki dunia huko kagera sugar........
MAMA MAGDARENA


MAMA VICTORIA

NJIWA WA KIJANI



Kipepeo victoria....mdogo wa maumbile na nikipenzi wa watu aliye mchangamfu







Kipepeo Magdarena mwenye rangi ya hariri msili asiependa bugudha




Njiwa wa kijani wavutia wengi baada ya kutinga katika viunga vya Bugango border....wakiwa safarini kwenda kusini mwa Afrika ...wakiamba na bonde la Ufa....wavinjari kwa makundi makubwa ya zaidi ya njiwa 300...500 yakubwa na inakadiriwa wanaizito karibu ya nusikilo kila mmoja....

Monday 27 May 2013

VIWANJA VYA MICHEZO KWA WATOTO WETU


WATOTO WAKUMBUKWE KIMICHEZO


>Viwanja vya michezo na sehemu za wazi ni huduma muhimu kwa jamii sehemu mbalimbali duniani.
Kwa muda mrefu jamii ya watu wa Tanzania imekuwa ikishiriki katika michezo mbalimbali katika makabila tofauti.
Kwa mfano kabla ya kuja wakoloni nchini, Watanzania walikuwa wakishiriki michezo mbalimbali katika makabila yao kama kucheza mieleka, kutupa mkuki, kulenga shabaha kwa upinde na mishale, sarakasi, kukimbia, kuruka, kuogelea na  kucheza bao.
Walipokuja wakoloni walituletea michezo ya kigeni kama soka, netiboli, ngumi, hoki, mpira wa kikapu, mpira wa wavu, tenisi, mpira wa meza, mpira wa mikono, kriketi, gofu, baiskeli na mingine mingi.
Ujio wa michezo hiyo ya kigeni nchini uliendana na ujenzi wa viwanja vya michezo hiyo na pia baada ya nchi yetu kupata uhuru Serikali ya awamu ya kwanza iliendelea kujenga viwanja vya michezo hiyo.
Serikali ya awamu ya kwanza iliendeleza viwanja na michezo hiyo ya kigeni kwa kuwa ilitambua michezo ni sehemu ya uhai na utashi wa taifa letu.
Ndiyo maana Tanzania ilipata mafanikio makubwa katika michezo kama soka, riadha, ndondi, netiboli na michezo mingine hasa katika awamu ya kwanza.
Tunasema hivyo kwa sababu tunafahamu Tanzania ilipata nafasi ya kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika katika soka kwa mara ya kwanza wakati Serikali ya awamu ya kwanza ikiwa madarakani.
Pia, Tanzania inajivunia kupata medali mbili tu za Olimpiki ambazo zote zilipatikana wakati wa utawala wa Serikali ya awamu ya kwanza.
Tunafahamu kwamba wakati wa utawala wa Serikali ya awamu ya pili ndipo viwanja vingi vya michezo vilibadilishwa matumizi yake, pia maeneo mengi ya wazi yalivamiwa. Hali hiyo iliendelea katika utawala wa Serikali ya awamu ya tatu na inaendelea mpaka katika utawala huu wa Serikali ya awamu ya nne.
Tunasikitika kuona Serikali imelifumbia macho tatizo la viwanja vya michezo nchini kuvamiwa na kubadilishwa matumizi yake, pia tunasikitika kuona Serikali haijengi viwanja mbalimbali vya michezo nchini.
Vilevile tunasikitishwa na Serikali kushindwa kuwazuia watu mbalimbali wasivamie maeneo ya wazi yaliyokuwa yametengwa kwa ajili ya watoto kuyatumia kwa michezo au watu kupumzika.
Tunashangaa kuona viongozi wa Serikali za mitaa, halmashauri na manispaa nchini wanashindwa kuelewa kuna ardhi ya biashara na ardhi ya jamii, lakini wamekuwa wakishindwa kusimamia ardhi ya jamii ambayo imekuwa ikichukuliwa kwa matumizi ya biashara au matumizi ya watu binafsi.
Kutokana na ardhi ya jamii kuvamiwa, Tanzania imekuwa na tatizo kubwa la viwanja vya michezo, maeneo ya wazi na maeneo ya kupumzika, hivyo kusababisha kukosa wanamichezo mahiri, vijana kukosa sehemu za kupumzika na hivyo kukimbilia kwenye baa na kumbi mbalimbali za starehe kwa ajili ya kupumzika.
Tunatarajia kuona Serikali na wizara zote zinazohusika na usimamizi wa ardhi ya jamii kuhakikisha ardhi ya jamii haivamiwi na watu wote waliovamia katika ardhi hiyo wanaondolewa.
Tunaamini ardhi ya jamii ni muhimu katika maendeleo ya jamii kwa sababu ardhi ya jamii inakuwa na viwanja vya  michezo, maeneo ya wazi, viwanja vya kupumzika, ambapo  watu huweza kukutana na kubadilishana mawazo huku, pia watu watafanya mazoezi na kuepuka maradhi mbalimbali ya mwili na kiakili......

PICHA ZA MATUKIO YA VURGU MTWARA

Tunaiombea Tanzania amani na upendo tuepushe haya yanayo endelea hiko mtwara
Yaliyo tokea Mtwara uharibifu wa majumba na mali za serekali
Mtaa ukiwa kimya kabisa wakati oparesheni ya kuwasaka walio fanya uharibifu Mtwara katika sakata la Gesi ya mtwara......vijana waki shanga wasijue nini la kufanya...

Mikusanyika ya vijana wasio na kazi wakitupa mawe na kufanya vurugu katika viunga vya Mtwara




Uchomaji wa matairi Barabarani wakati barabara zikiwa hazina watu hata mmoja wakihofia kukamatwa na askari walinda amani mjini Mtwara


Nidhahiri uharibifu ulikuwa mkubwa katika viunga vya mji wa Mtwara ...uharibifu uliotendwa nidhahili sisi walipakodi na kuhalibiwa mali za serikali tunao umia ni sisi wafanyakazi tunao lipa kodi

ZIARA YA RAISI KIKWETE

RAIS KIKWETE AKUTANA NA MARAIS WASTAAFU, AHUDHURIA KIKAO CHA AMANI DRC CONGO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizingumza na Marais Wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Mzee Benjamin Mkapa na Waziri Mkuu Mstaafu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Afrika Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim kuhusiana na sherehe za miaka 50 ya AU alipokutana nao jijini Addis Ababa, Ethiopia, leo  Mei 26, 2013. Viongozi hao wastaafu ni miongoni mwa wageni mashuhuri walioalikwa kwenye sherehe hizo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na wanahabari baada ya kuhudhuria Mkutano wa Kanda wa Usimamizi wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika DRC na nchi za Maziwa Makuu katika makao makuu ya Umoja wa .
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika  Mkutano wa Kanda wa Usimamizi wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika DRC na nchi za Maziwa Makuu katika makao makuu ya Umoja wa Afrika leo 
About these ads