Saturday 22 June 2013

Alichokisema bungeni

Nchemba, Msigwa nusura 

wazichape Dodoma


msigwa
Dodoma. Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa na mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba jana nusura wachapane makonde baada ya kutupiana maneno ya kashfa, wakituhumiana kuhusika na mlipuko wa bomu uliotokea Jumamosi iliyopita mkoani Arusha.
Tukio hilo lilitokea katika viwanja vya Hoteli ya St Gasper nje kidogo ya mji wa Dodoma, walipokwenda kwa ajili ya kuhudhuria semina ya wabunge wapambanaji na Ukimwi, ambapo baadhi ya wabunge wa Chadema walihudhuria, baada ya kutoonekana mjini humo tangu Juni 17 mwaka huu.
Wabunge hao wa Chadema hawakuhudhuria kikao chochote cha Bunge kutokana na kwenda mkoani Arusha kwa shughuli mbalimbali, kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea katika mkutano wao wa kuhitimisha kampeni zake za uchaguzi mdogo wa udiwani katika viwanja vya Soweto, Juni 16 jijini humo.
Malumbano hayo yanatokana na Nchemba kuituhumu Chadema kuhusika na mlipuko huo, Juni 20 mwaka huu wakati akichangia hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2013/2014, akisema chama hicho kilipanga kulipua bomu hilo ili kuwafanya Watanzania waamini kuwa Serikali ya CCM ndiyo inayohusika na tukio hilo.
Ilivyotokea
Wakati Msigwa akiingia katika ukumbi huo akiwa ameongozana na Mbunge wa Nyamagana (Chadema), Ezekiah Wenje, walikutana uso kwa uso na Nchemba ambaye alikuwa akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Said Amour Arfi.
Baada ya Nchemba kumwona Msigwa alimkaribisha mchungaji huyo akisema; “Karibu sana bwana, salama lakini?”
Hata hivyo, badala ya kujibu salamu hiyo ya Nchemba, Msigwa alikuja juu na kumtuhumu Nchemba kwamba anatoa kauli zinazoweza kuvuruga amani ya nchi.
“Wewe ni mtu hatari sana, haya yote yanasababishwa na wewe, mnatumia damu za watu kutafuta madaraka,” alisema Msigwa akimtupia maneno Mwigulu.
Baada ya kauli hiyo Nchemba alihoji akisema: “Ki-vipi? Hayo mambo tuyaache, Msigwa achana na haya mambo!”
Baada ya Nchemba ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM kujibu, Msigwa alimsogelea karibu na kumnyooshea kidole, huku akiendelea kumtuhumu kuwa ana siasa chafu zinazopandikiza chuki kwa jamii.
Malumbano hayo pia yaliingiliwa na Mbunge wa Musoma Mjini (Chadema), Vicent Nyerere ambaye alimuunga mkono Msigwa, huku akimtuhumu Nchemba kuwa ni mtu mbaya katika siasa za Tanzania. Katika kile kilichoonekana kutaka kuweka mambo sawa, Wenje alimvuta Msigwa na kumpeleka ukumbini ili kuepusha shari baada ya wabunge hao kuzidi kurushiana maneno.
Hata walipoingia ndani ya ukumbi huo wabunge hao waliendelea kulumbana, lakini wakatulizwa na baadhi ya wabunge waliokuwa karibu yao.
Alipotakiwa kueleza sababu za mzozo huo na Nchemba, Mchungaji Msigwa alisema, “Achana na yule mpuuzi, mimi siwezi kuzungumza na mtu mnafiki, mkatili na yeye ndiye alihusika na mipango mibaya dhidi ya Chadema hata mlipuko wa Arusha hivyo kutesa watu wa Chadema.”
Alisema kuwa yeye haoni sababu ya mtu mwenye mipango mibaya na wananchi wa Tanzania pamoja na chama chake (Chadema), kuwafuata na kujikomba.
Kwa upande wake Nchemba alipoulizwa alisema kuwa alichokizungumza ni mtazamo wake na kwamba ikiwa kuna mtu anayeona kuwa alizungumza uzushi, ajitokeze na kupinga. “Nilichokizungumza ndicho kilichofanyika kwa matukio yote niliyoeleza bungeni,”alisisitiza Nchemba.
Alichokisema bungeni

Wakati akichangia mjadala wa Bajeti, Nchemba alisema hata ripoti iliyotolewa na Jukwaa la Wahariri baada ya kutekwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Absalom Kibanda, ilieleza kuwa watu waliohojiwa walidai kuwa Chadema kimepewa mafunzo kutoka nje ya nchi, kwamba kikitumia baadhi ya viongozi wa dola wasiokuwa waaminifu kuteka watu na hata kuua watu maarufu, watu wataamini CCM imeshindwa kuongoza nchi na sasa imeanza kuua watu.

Akizungumzia mkanda wa video unaoonyesha tukio la mlipuko wa bomu la Arusha, Nchemba alisema kuwa tukio hilo lilipangwa na ndiyo maana Chadema walipanga hadi wakarekodi tukio hilo.
“Lile tukio limepangwa na ndiyo maana hata aliyechukua ile video hakustushwa kabisa na mlipuko wa bomu, jambo hilo haliwezekani kabisa, tukio lile limepangwa kwa kiwango cha chini kabisa,” alisema na kuongeza; “Mtu yule alikuwa akichukua video utadhani yuko katika harusi,
CCM haijashiriki katika tukio la Arusha, ila kutokana na nguvu ya chama hiki ni lazima kitahusishwa na tukio hilo.”

Elikana, Eliud;....Watoto walioungana

Elikana, Eliud; Watoto walioungana wanaotumia njia moja kujisaidia

 

Madaktari waliponiambia kuwa watoto wangu wameungana nilichanganyikiwa, niliona dunia imenigeuka, sikuwahi kuwaza nitakutana na kitu cha namna hii katika maisha yangu.
Ni maneno ya binti kutoka Mbeya, Grace Joel (19), ambaye Februari 20 mwaka huu, alijifungua pacha wa kiume ambao wameungana katika sehemu ya kiunoni.
Mwanadada huyo anasema hakuamini macho yake pale madaktari wa Hospitali ya Uyole iliyopo mkoani humo walipomwambia kuwa watoto wake wameungana na hivyo kupewa rufaa ya kwenda kwenye Hospitali Kuu ya Mkoa wa Mbeya.
Wakati wa ujauzito wangu sikuwahi hata siku moja kuhisi kuwa ningeweza kuzaa watoto wakiwa kwenye tatizo hili, sikuwahi kuumwa zaidi ya kuvimba miguu tu na hiyo ni hali ya kawaida kwa mjamzito yeyote. anasema Grace ambaye kwa sasa anahitaji msaada wa hali na mali ili kuokoa maisha ya watoto wake.
Licha ya umri huo mdogo, amejikuta kwenye hali ya mateso na uchungu mwingi baada ya familia yake, hususani mume wake, Erick Mwakyusa kumtelekeza kwa kile alichodai kuwa hana haja na watoto walioungana.
Nilishangaa, familia yangu kunitelekeza katika hali hii baada ya kugundua watoto wameungana, mume na familia yake alinitamkia wazi kuwa hawana shida na watoto walioungana, alisema hawezi kuwalea kwa kuwa kwao hakuna watoto wenye ulemavu wa aina hiyo, anasema.
Siyo siri nilijisikia uchungu, sikuamini kuwa mume wangu angenifanyia hivyo, siyo yeye tu hata familia yao yote sikudhani kama wangenigeuka hivyo, nashukuru kwa upande wa familia ya wazazi wangu walikuwa pamoja nami ingawa ni maskini na hawana uwezo wa kunisaidia.
Hospitali ya Kyela ndiyo iliyonipeleka ile ya Rufaa Mbeya ambao nao walivyoona hali ya watoto wangu wakanishauri kuja Muhimbili, sikuwa na uwezo wa kufika hapa, lakini nawashukuru madaktari wa Rufaa Mbeya walioniwezesha kufika hapa.
Grace anasema watoto wake hao, Elikana na Eliud aliwazaa wakiwa na uzito kilo tano na nusu na walifika Hospitali ya Taifa Muhimbili wiki mbili tangu kuzaliwa kwao.
Wanatumia njia moja kujisaidia
Dk Zaituni Bokhari, ambaye ni Daktari Bingwa katika Kitengo cha Upasuaji kilichopo Hospitali ya Taifa Muhimbili, anasema kutokana na namna walivyoungana, wanatumia njia moja kujisaidia.
Njia ya kukojolea wanatumia moja na pia njia ya haja kubwa wanatumia moja, tutakapowatenganisha kuna utaalam ambao utafanywa ili kila mtu aweze kutumia njia yake mwenyewe bila athari zozote, anasema.
Anaeleza kwamba, iwapo upasuaji huo utafanikiwa watoto hao watakuwa kule India kwa wiki mbili ndipo watarejea nchini na kuendelea na matibabu chini ya uangalizi wa wataalamu wa Hospitali ya Muhimbili hadi pale afya zao zitakapoimarika.
Kutokana na hali ya kiuchumi ya mama huyo, Dk. Bokhari amewataka wasamaria wema kujitokeza na kutoa misaada mbalimbali kama ya maziwa, nguo na fedha kwa ajili ya vitu vidogo vidogo ili aweze kuwahudumia vyema watoto wake.
Dk. Bokhari anasema wao waliwapokea watoto hao wakiwa katika hali mbaya kutokana na uchovu wa safari kwa basi kutoka Mbeya na walikuwa na maambukizi sehemu mbalimbali.
Walikuwa ni wachanga kabisa, walikuwa na wiki mbili, walikuwa wamechoka kutokana na mwendo mrefu wa basi kutoka Mbeya, walikuwa na homa kali na matatizo katika njia ya kupumua, tukatibu kwanza matatizo hayo ndiyo vipimo vingine vikaendelea, anasema.
Wamefika hapa hawakuwa hata na nguo za kutosha, huyu mama naye alikuja katika hali ya kuchanganyikiwa ukizingatia ukweli kuwa ndugu zake wamemtelekeza, tumefanya kazi kubwa sana ya kumpa ushauri nasaha mpaka akakubaliana na hali halisi.
Kuna wakati alikuwa anasema anataka kuondoka awaache watoto kwetu, hali hiyo ilitokana na kuchanganyikiwa, muda mwingi alikuwa akilia ila kwa sasa namshukuru Mungu yeye na watoto wanaendelea vizuri, anasema.
Kwa nini wameungana
Dk Bokhari anasema hali ya watoto kuungana siyo ya kurithi kama yalivyo kwa baadhi ya magonjwa.
Hali hii inaweza kusababishwa na upungufu wa madini, anaeleza.
Mtaalamu mwingine wa afya ameliambia gazeti hili kuwa, Pacha wanaofanana kwa kawaida hutokana na yai lililopandikizwa kujigawa mara mbili, baada ya siku 12 mgawanyiko wa seli (chembe chembe) unakuwa umeanza kujipanga kwa ajili ya kujiachanisha katika uumbwaji wa viungo au ogani mbali mbali za mwili.
Anasema kuwa, jinsi siku zinavyozidi kusogea mgawanyiko wa mapacha kujiachanisha na kujitegemea ikitokea kabla ya seli kufikia wakati wa kuruhusu jambo hilo, ngozi nyembamba za mapacha hao huendelea kuungana na kushikamana.
Hata hivyo kwa sayansi ya tiba chanzo kikuu hasa hakijulikani, anaeleza mtaalam huyo.
Matibabu ni India pekee?
Dk Bokhari anasema kutokana na aina ya upasuaji wa watoto hao, inabidi ufanyike kwenye nchi zenye watalaamu na vifaa vya kisasa kama India au Afrika Kusini.
Upasuaji huu unatakiwa ufanywe na madaktari zaidi ya saba na kila daktari atakabiliana na kiungo chake, mimi pia ni miongoni mwa madaktari ambao nitashiriki upasuaki wa watoto hawa na inatakiwa umakini wa hali ya juu, anasema.
Anaeleza kuwa, upasuaji wa aina hiyo unaweza kufanyika kwa saa 24 ama chini ya hapo.

Friday 21 June 2013

Mke wa Rais wa Marekani,


Mke wa Rais wa Marekani,

Michelle Obama,

“Ni wale wa nchi za Afrika ambao watajumuika na mke wa Rais mstaafu wa marekani George W Bush na mke wa Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Cherly Blair”

Dar es Salaam. Rais wa zamani wa Marekani, George W. Bush na mkewe,Laura wanatarajiwa kuendesha Mkutano wa Kimataifa wa wake wa marais wa Afrika kuzungumzia nafasi ya wanawake kuinuka kimaendeleo utakaofanyika Dar es Salaam, Julai 1-2 mwaka huu.

Mkutano huo ambao ni wa kwanza kufanyika nchini, utakwenda sambamba na ziara ya Rais wa Marekani, Barack Obama pia utajumuisha maofisa wa Serikali,viongozi wa mashirika ya kiraia na wasomi wa kada mbalimbali.Taarifa iliyotolewa na Wakfu wa George W. Bush imesema kuwa mkutano huo utakaokuwa na kauli mbiu; “Kuwekeza kwa wanawake kunaiinua Afrika” imewataja baadhi ya wazungumzaji kuwa ni pamoja na Bush mwenyewe na mkewe Laura, Mke wa Rais wa Marekani,Michelle Obama, Mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza,Cherie Blair na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Ukimwi (Unaids), Michel Sidibé.

Taarifa hiyo imesema kuwa wake hao wa marais wa Afrika wanatoa mchango mkubwa wa kusukuma mbele agenda za maendeleo katika sekta za afya na elimu hivyo kukutana kwao kutatoa fursa nyingine ya kujadiliana changamoto zinazowakabili na kuweka mikakati ya pamoja.

“Wake za marais wanalo jukumu muhimu kuhusiana na uboreshwaji wa ustawi wa wanawake… wao wana nafasi kubwa ya kuinua na kuboresha sekta kama elimu,afya na maendeleo ya kiuchumi hivyo kukutana kwao ni hatua muhimu itayotoa mwanga kuhusiana na hatua zinazopaswa kufanywa kuwawezesha wanawake,”ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Baadhi ya wake za marais watakaohudhuria mkutano huo ni wa pamoja na Mke wa Rais wa Uganda, Janet Museveni,mke wa Rais wa Msumbiji, Maria da Luz Dai Guebuza, mke wa Rais wa Sierra Leone, Sia Nyama Koroma na mwenyeji wao Salma Kikwete.

Miongoni mwa mada zinazotarajiwa kujadiliwa wakati wa mkutano huo ni pamoja na kuwawezesha wanawake ujasiriamali kupitia mafunzo ya teknolojia,kutoa fursa na kuboresha shughuli za kilimo kwa wakulima wanawake na ukoaji wa maisha kwa kukabiliana na saratani ya ziwa.

SELEKALI IMECHOSHWA NA UTUKUTU WETU SISI WANASIASA


SELEKALI IMECHOSHWA NA UTUKUTU
WETU SISI WANASIASA

Amani si kitu cha mchezo
 
JIHESHIMU UHESHIMIKE …..AMANI YA TANZANIA  ITALINDWA KWA NJIA ZOZOTE ZILE
Kupitia kauli ya wazili wetu mkuu alivyo tuasa, mimi nafikiria ni moja ya maaso ya mwisho kwa mtu mzima aidha alie choshwa na utukutu wetu sisi wana siasa ambao bado tume nga’nga’nia kushikilia mna kuabudu uana siasa wa kizamani wa kutukanana kushabikia vurugu mauaji na hata kuunda chuki ndani ya jamii na kuwaacha matajili wetu ambao ni wananchi tunao washawishi kutuchagua tuingie katika mchakato wa kutuwakilishia madai ,
matakwa yetu huko Mjengoni(BUNGENI) sasa mchakato huo unakuja katika picha hii inayo toa picha mbaya yenye kututia kichefu chefu sisi wananchi kwakweli na sisi sasa tunaona ni vyema kwa kauli ya wazili mkuu aliyo itoa huenda ikawa na uzito na yenye kututia uchungu sana sisi wananchi……kila kukicha kuna jitokeza kauli katika vyombo vya habari na tunasikia yaliyo jiri katika anga la walalahoi ambao ndio wanao ombwa kura kwa vipigo, kudharirishwa, kuchaniwa mavazi yao waliyo yanunua  kwa shida ….pia mabomo nayo hayako nyuma yanapenya mpaka ndani ya vyumba vyetu na yakitudhuru sisi wapenda amani,  wakezetu watoto wetu pia wajukuu zetu kwetu sisi wananchi tupendao amani na eti kisa ni wanasiasa wanaowania kwenda mjengoni (BUNGENI) au UDIWANI hivi huko mjengoni (BUNGENI) au ADIWANI hivi himo mjengoni BUNGENI  kutakuwa eneo la kudaiwa hakizetu za maendeleo sisi walalahoi  au litakuwa  eneo la kutekeleza vyisasi, kukomoana, kuzushiana chuki baina ya serekali, wananchi ambao ndio walala hoi, wabunge wenye kuitakia meme walalahoi wa Taifa hili la Tanzania ambalo… lilikuwa Taifa lenye amani utulivi, humu duniani sasa basi WAZILI WETU MKUU KASEMA hakuna mjadala, mjadala tutaupata kwa wahusika watakao lishughulikia hili jee? na tukiwa sisi wapenda amani tutatii maagizo ya serekali na kudai haki zetu kwa ustarabu au tusubili kichapo kutoka kwa wadogo zetu, watoto wetu na hata wajukuu zetu

“WATANZANIA TUJIUNGENI  PAMOJA KUYAKEMESAHA HAYA YANAYO ENDELEA KATIKA KULIGAWA TAIFA LETU HILI AMBALO NI KISIWA CHA AMANI”

Thursday 20 June 2013

Uwanja wa Soweto....wawaka moto



 Uwanja wa Soweto....wawaka moto


Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) pamoja na askari kutoka Chuo cha Mafunzo ya Polisi (CCP) Moshi wakiwa kwenye Uwanja wa Soweto, Arusha kuwadhibiti waombolezaji waliofika kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa watu watatu waliopoteza maisha kwenye mlipuko wa bomu uliotokea Jumamosi iliyopita. Picha na Filbert Rweyemamu 

Kubwa zaidi ni kifo cha mtoto Amir Ally (7) anayedaiwa kupigwa risasi na polisi. Maelezo ya kifo cha Ally yamenukuliwa kutoka kwa mtoto mwenzake Abubakar Adam (11), ambaye amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru akiuguza majeraha yanayodaiwa kutokana na risasi.
Jumamosi ya Juni 15, 2013 Jiji la Arusha kwa mara ya pili ndani ya kipindi kifupi liliendelea kuandika historia ya hatari kwa kutokewa na vitendo vya kigaidi. Vitendo vya kurusha mabomu kwenye mikusanyiko ya watu na kusababisha maafa.
Tukio la kwanza lilitokea Mei 5, 2013, katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasit mjini Arusha na kusababisha vifo vya watu watatu. Tukio hilo kwa sasa kesi yake iko mahakamani.
Hata hivyo tukio la Jumamosi iliyopita lilitokea kwenye Uwanja wa Soweto mjini Arusha wakati wa mkutano wa kukamilisha kampeni za udiwani wa Chadema. Wasiwasi mkubwa ulizuka katika tukio hilo ni kuhusishwa polisi na vifo vilivyotokea.
Kubwa zaidi ni kifo cha mtoto Amir Ally (7) anayedaiwa kupigwa risasi na polisi. Maelezo ya kifo cha Ally yamenukuliwa kutoka kwa mtoto mwenzake Abubakar Adam (11), ambaye amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru akiuguza majeraha yanayodaiwa kutokana na risasi.
Licha ya hao wawili, Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Arusha Medical Lutheran Center (ALMC), Dk Paul Kisanga aliwataja watoto wengine wawili ndugu Fatuma na Sharifa Jumanne ambao wamepelekwa Nairobi, Kenya, kwa matibabu zaidi baada ya miili yao kukutwa na vyuma.
Dk Kisanga alimtaja mtoto mwingine Fahad Jamal (7) ambaye yuko chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU), akisubiri timu ya madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Kwa mujibu wa Dk Kisanga watoto hao watano walipatwa na matatizo hayo wakati wakitoka madrasa eneo la Kaloleni (Madrasa ni shule zinatoa elimu ya dini ya Kiislamu), iliyopo jirani na Uwanja wa Soweto.
Tukio la Soweto limekuwa na matukio mawili ndani yake; kwanza ni tukio la kurushwa bomu ambalo mtuhumiwa wake hajafahamika, tukio la pili ni matumizi ya silaha za moto ambazo sababu za matumizi yake na wahusika bado ni kitendawili.
Hata hivyo, mashuhuda wa tukio hilo akiwamo mtoto Amir Ally wanadai polisi walipiga risasi watu, wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kudai kuwa mtuhumiwa wa bomu hilo alionekana akisafirishwa na gari pale wananchi walipotaka kumvamia.
Wakuu wa polisi kwa upande wao wamekiri kupatikana kwa maganda ya risasi katika eneo la tukio, hii ina maanisha kwamba ni kweli ndani ya tukio la ulipuaji bomu kulikuwa na tukio lingine la ufyatuaji risasi. Lakini bado hakujawa na ushahidi wa moja kwa moja kwamba nani alifyatua risasi na kwa sababu gani. Madai ya kufyatulia risasi watoto yana uzito wa pekee, pamoja na kutokuwepo kwa ushahidi wa moja kwa moja, vidole vingi vimekuwa vikinyooshwa kuwatuhumu polisi, kwamba risasi zilizofyatuliwa eneo la tukio zilitoka kwa polisi, na watoto walipigwa risasi na polisi.



Hata hivyo, Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema tayari ameunda timu ya askari polisi kuchunguza tukio hilo ambalo polisi wanatuhumiwa.
Kwanza tuweke wazi kwamba tuna imani kubwa na utendaji kazi wa Jeshi Polisi, hivyo maoni yetu ni katika kujenga nyumba moja kwa maana tukio la Soweto kwa watoto kupigwa risasi linahitaji Tume Huru itakayokuwa na kada mbalimbali za wataalamu.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) pamoja na askari kutoka Chuo cha Mafunzo ya Polisi (CCP) Moshi wakiwa kwenye Uwanja wa Soweto, Arusha kuwadhibiti waombolezaji waliofika kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa watu watatu waliopoteza maisha kwenye mlipuko wa bomu uliotokea Jumamosi iliyopita. Picha na Filbert Rweyemamu 

Kubwa zaidi ni kifo cha mtoto Amir Ally (7) anayedaiwa kupigwa risasi na polisi. Maelezo ya kifo cha Ally yamenukuliwa kutoka kwa mtoto mwenzake Abubakar Adam (11), ambaye amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru akiuguza majeraha yanayodaiwa kutokana na risasi.Tunaamini kuwa hata kama tume iliyoundwa na Mwema itafanya kazi yake kwa uadilifu mkubwa, bado hali ya wasiwasi itaendelea kuwapo kwa kuwa polisi wananyooshewa kidole karibu na watu wengi. Ni vyema Serikali ingeunda Tume Huru.