Saturday 10 August 2013

BILAL : TUKATAE KUGAWANYWA KWA MISINGI YA DINI

BILAL : TUKATAE KUGAWANYWA KWA MISINGI YA DINI

Akizungumza katika Baraza la Eid El Fitr mjini Tabora jana, Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal amesema “ni busara waumini wa dini na madhehebu kujenga utamaduni wa kuvumiliana hasa  zinapotokea hitilafu miongoni na kati yao. Ubaguzi unaotokana na kabila, rangi, jinsia au mahala mtu alipo au anapotoka nii lazima kuukemea na kuukataa kwa nguvu zetu zote.”.

“Kaeni pamoja na kutafuta muafaka kwa njia ya majadiliano ya amani na upendo, pasipo kutawaliwa na jazba wala chuki. Tukumbuke kauli na angalizo la Rais Jakaya Kikwete kwamba vita ya dini haina mshindi,” alisema.

Alisema anaamini viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kusaidia kujenga maadili mema katika taifa hili na kwamba watu wakishiba imani ndani ya nafsi zao, wakaelewa na kuzingatia mafundisho ya dini zao, maovu yataondoka kati yao.

Aidha Dr. Bilal alisema “kuwepo kwa amani na utulivu unaifanya serikali kupata ahueni, kwamba badala ya kutenga bajeti   kubwa kupanua magereza, kugharamia wafungwa na mahabusu na uendeshaji wa mahakama, rasilimali hizo zitaelekezwa katika mipango mingine ya maendeleo.”
 
Dk. Bilal alisema katika siku za hivi karibuni, yameibuka matukio kadhaa yanaoashiria kutaka kuvuruga amani na utulivu wa taifa na kwamba hujuma hizo zinafanywa na watu wachache wasiolitakia mema taifa kwa maslahi yao binafsi.

Aliongeza kuwa “kamwe serikali haitakuwa tayari kuona Mtanzania anaishi kwa hofu na mashaka ndani ya nchi yake kutokana na vitendo vya wahuni wachache. Kila itakapobidi, tutawasaka, tutawakamata na kuwakomesha kwa rungu la mkono wa sheria. Nawahakikishieni kwamba Tanzania yetu itabaki nchi salama ya amani na utulivu na ya kupigiwa mfano daima.”

Alisema uhuru wa kuabudu katika taifa hili umejengewa misingi ndani ya katiba na kutokana na ukweli huo, kila mmoja anapaswa kuheshimu imani au dini ya mwenzake pasi kujiona kwamba imani au dini yake ni bora zaidi.BILAL : TUKATAE KUGAWANYWA 
KWA MISINGI YA DINI

 
 
 
 
Akizungumza katika Baraza la Eid El Fitr mjini Tabora jana, Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal amesema “ni busara waumini wa dini na madhehebu kujenga utamaduni wa kuvumiliana hasa zinapotokea hitilafu miongoni na kati yao. Ubaguzi unaotokana na kabila, rangi, jinsia au mahala mtu alipo au anapotoka nii lazima kuukemea na kuukataa kwa nguvu zetu zote.”.

“Kaeni pamoja na kutafuta muafaka kwa njia ya majadiliano ya amani na upendo, pasipo kutawaliwa na jazba wala chuki. Tukumbuke kauli na angalizo la Rais Jakaya Kikwete kwamba vita ya dini haina mshindi,” alisema.

Alisema anaamini viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kusaidia kujenga maadili mema katika taifa hili na kwamba watu wakishiba imani ndani ya nafsi zao, wakaelewa na kuzingatia mafundisho ya dini zao, maovu yataondoka kati yao.

Aidha Dr. Bilal alisema “kuwepo kwa amani na utulivu unaifanya serikali kupata ahueni, kwamba badala ya kutenga bajeti kubwa kupanua magereza, kugharamia wafungwa na mahabusu na uendeshaji wa mahakama, rasilimali hizo zitaelekezwa katika mipango mingine ya maendeleo.”

Dk. Bilal alisema katika siku za hivi karibuni, yameibuka matukio kadhaa yanaoashiria kutaka kuvuruga amani na utulivu wa taifa na kwamba hujuma hizo zinafanywa na watu wachache wasiolitakia mema taifa kwa maslahi yao binafsi.

Aliongeza kuwa “kamwe serikali haitakuwa tayari kuona Mtanzania anaishi kwa hofu na mashaka ndani ya nchi yake kutokana na vitendo vya wahuni wachache. Kila itakapobidi, tutawasaka, tutawakamata na kuwakomesha kwa rungu la mkono wa sheria. Nawahakikishieni kwamba Tanzania yetu itabaki nchi salama ya amani na utulivu na ya kupigiwa mfano daima.”

Alisema uhuru wa kuabudu katika taifa hili umejengewa misingi ndani ya katiba na kutokana na ukweli huo, kila mmoja anapaswa kuheshimu imani au dini ya mwenzake pasi kujiona kwamba imani au dini yake ni bora zaidi.

Friday 9 August 2013

MAAGIZO YA Dr. Rais Kikwete Yaitikiwa asilimia %99



Rwanda yamjibu 

Rais Kikwete


Dar. Serikali ya Rwanda imetoa tamko linaloonyesha kutoielewa kauli ya
Rais Jakaya Kikwete, iliyoamuru wahamiaji haramu kuondoka nchini, hali inayoonekana kukwepesha hoja.
Rwanda kupitia waziri wake wa Mambo ya Nje, Louise Mushikiwabo, ilikaririwa ikieleza kwamba hawatajibu mapigo agizo la Rais Jakaya Kikwete ya kuwataka Wanyarwanda wote waliolowea Magharibi mwa Tanzania kuondoka haraka.
Mushikiwabo alisema wako tayari kuwapokea na kuwalinda wote waliofukuzwa Tanzania kwa kisingizio kuwa ni wahamiaji haramu, akieleza kwamba anasikitishwa kwa kuwa Tanzania haikufanya jitihada yoyote kuwasiliana na Rwanda kuhusu suala hilo kabla ya kuchukua uamuzi huo.
“Ni uamuzi ambao umeshachukuliwa, hatukushirikishwa kwa namna yoyote na jukumu letu kama serikali na taifa ni kuwahakikishia ulinzi wote wanaokuja, na hili ndilo suala tunalolishughulikia kwa sasa,” alisema.
Kwa mujibu wa gazeti la New Times, Mushikiwabo aliwaeleza waandishi wa habari kwamba agizo hilo la Rais Kikwete pamoja na ushauri wa kuitaka Serikali ya Rwanda kuzungumza na wanamgambo hasimu wa FDLR waliopo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), hayatayumbisha uhusiano imara baina ya Watanzania na Wanyarwanda.
“Sisi si majirani tu, tuna mfungamano imara baina ya watu wetu pia, tuna mfungamano wa damu, wa kibiashara, na mengine mengi ya kutufanya tuendelee kuwa pamoja,” alisema na kutumia fursa hiyo kuwakaribisha Watanzania nchini Rwanda.
Watanzania wanaweza kuishi hapa kwa umri wowote wanaotaka. Tunawachukulia kuwa ni watu wetu muhimu kwenye fungamano la Jumuiya ya Afrika Mashariki,” alisisitiza.
Rais Kikwete wakati akihitimisha ziara yake mkoani Kagera alitoa agizo la kuwataka wanaomiliki silaha kinyume cha sheria na wahamiaji haramu ama kuondoka au kuhalalisha ukazi wao, huku akitoa wiki mbili kwa zoezi hilo kutekelezwa, kabla ya kuanza kwa operesheni ya kuwasaka watu hao.
Kauli hiyo ilitokana na kushamiri vitendo vya kihalifu katika eneo la Kanda ya Ziwa, Rais hakutaja jina la nchi ya wahamiaji hao. Kwa ukanda huo Tanzania inapakana na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na DRC.
Pia, Rais Kikwete katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi alizungumzia kusikitishwa na kauli za shutuma, kejeli na udhalilishaji zilizotolewa na Rais Paul Kagame wa Rwanda dhidi yake.
Mvutano baina ya Rwanda na Tanzania ulianza kuwekwa hadharani Mei mwaka huu, baada ya Rais Kikwete kuishauri Rwanda kukaa na kuzungumza na FDLR wenye makao yao DRC, hatua ambayo haikuifurahisha Serikali ya Rwanda.
Wakati Rwanda ikieleza hayo jana Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue alizungumza na gazeti hili, na kutaka majibu ya kauli hiyo ya Rwanda yatolewe na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Mkumbwa Ally alisema kauli iliyotolewa na Rais Kikwete ilikuwa ni ushauri, kwamba Rwanda wanaweza kuukubali ama la.
“Kilichomkasirisha Rais Kikwete ni lugha za matusi zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa Rwanda, ila kwa hicho walichokisema sidhani kama kitakuwa na tatizo kwetu,” alisema Mkumbwa.
Alifafanua kwamba, alipokuwa mkoani Kagera Rais Kikwete hakutoa agizo la Wanyarwanda kufukuzwa, bali alitoa agizo la kuanza kwa operesheni ya kuwakamata wahamiaji haramu, wale wanaomiliki silaha kinyume na taratibu.
“Rais alizungumzia masuala ya jinai ‘Criminal Element’, siyo kuwafukuza Wanyarwanda,” alisisitiza.
Hatutazungumza na FDLR
Waziri wa Mambo ya Nje, Louise Mushikiwabo, aliendelea kusema sera ya Rwanda kuhusiana na makundi ya aina hiyo, iko wazi na haitabadilika, kauli ambayo amekuwa akiirudia kila mara na kuwataka wote wanaofikiria kuhusu Rwanda kuzungumza na FDLR kwa namna yoyote kusahau wazo hilo.
“Kama umehusika kwa namna yoyote na maangamizi, wewe utakuwa adui wa kila mtu. Ni wazi kwamba Wanyarwanda wote watakuwa kwenye majonzi iwapo kwa namna yoyote kutakuwa na mawasiliano ya FDLR,” alifafanua.
Kundi la FDLR ambalo ni kifupisho cha Democratic Forces for the Liberation of Rwanda, linaundwa na watu walioshiriki kwenye mauaji ya kimbari yaliyowalenga watu wa kabila la Watutsi mwaka 1994, na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 800,000 kwa miezi mitatu.
Kundi hilo ambalo limeweka makazi yake mashariki mwa DRC, linadaiwa kufanya mashambulizi kadhaa yakiwamo ya milipuko ya mabomu nchini Rwanda, ambapo mwezi uliopita shambulio la aina hiyo mjini Kigali lilisababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi watu kadhaa.
Uhusiano wa kihistoria
Familia za Rwanda zikiwamo zilizoishi Tanzania tangu miaka ya 1950, zimeelezwa kuwa zimekuwa zikiwasili nchini humo kupitia mpaka wa Rusumo baada ya agizo la Rais Kikwete kuwataka wawe wameondoka ndani ya wiki mbili, kabla ya kuanza kwa operesheni rasmi ya kuwaondoa.
Kwa mujibu wa mamlaka nchini Rwanda, mamia ya Wanyarwanda waliokuwa wakiishi mkoani Kagera ambako ndiko Tanzania inapopakana na Rwanda wamekuwa wakirejea kwa wingi, ambapo hadi juzi, zaidi ya watu 300 walikuwa wameshaorodheshwa kwenye ofisi za Uhamiaji.

RAIA WA RWANDA WAENDELEA KURUDI MAKWAO

RAIA WA RWANDA WAENDELEA KURUDI MAKWAO

Ofisa Uhamiaji wa Kituo cha Rusumo, Samweli Mahirane amethibitisha kuwa hadi sasa zaidi ya Wanyarwanda 500 kutoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Ngara wamevuka mpaka kurejea makwao kutii agizo la Mheshimiwa Rais Dr. Jakaya Kikwete la kuwataka  wahamiaji haramu warejee makwao kwa hiari au wafuate taratibu za kuhalalisha uhamiaji wao kndani ya muda alioutoa.

Mahirane alisema wahamiaji hao wanatokea katika vijiji vya Wilaya za Ngara, Karagwe, Kyerwa, Biharamulo na Geita pamoja na Runzewe na wamekuwa wakiishi katika maeneo hayo bila vibali halali.

“Kuondoka kwa hiari kwa wahamiaji haramu, kutahitimishwa Jumatatu Agosti 12 na baada ya tarehe hiyo, vyombo vya dola vitaanza kufanya kazi kama agizo la Rais Kikwete lilivyoelekeza katika Mikoa ya Kagera na Kigoma,” alisema Mahirane.RAIA WA RWANDA WAENDELEA KURUDI MAKWAO

Ofisa Uhamiaji wa Kituo cha Rusumo, Samweli Mahirane amethibitisha kuwa hadi sasa zaidi ya Wanyarwanda 500 kutoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Ngara wamevuka mpaka kurejea makwao kutii agizo la Mheshimiwa Rais Dr. Jakaya Kikwete la kuwataka wahamiaji haramu warejee makwao kwa hiari au wafuate taratibu za kuhalalisha uhamiaji wao kndani ya muda alioutoa.

Mahirane alisema wahamiaji hao wanatokea katika vijiji vya Wilaya za Ngara, Karagwe, Kyerwa, Biharamulo na Geita pamoja na Runzewe na wamekuwa wakiishi katika maeneo hayo bila vibali halali.

“Kuondoka kwa hiari kwa wahamiaji haramu, kutahitimishwa Jumatatu Agosti 12 na baada ya tarehe hiyo, vyombo vya dola vitaanza kufanya kazi kama agizo la Rais Kikwete lilivyoelekeza katika Mikoa ya Kagera na Kigoma,” alisema Mahirane.

Wanyarwanda 520 watii agizo




Wanyarwanda 520 watii agizo la Kikwete kuondoka nchini





Bukoba. Ngara. Zikiwa zimesalia saa 48 kabla ya kumalizika kwa muda uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwa wahamiaji haramu kuondoka nchini au kuhalalisha ukaazi wao na wenye silaha kuzisalimisha, makundi ya wahamiaji hao, yameanza kuondoka kwa hiari.
Wastani wa wahamiaji haramu 150 wanaendelea kujiandikisha kuvuka mpaka katika Kituo cha Rusumo, Ngara mkoani Kagera kutekeleza agizo hilo.
Ofisa Uhamiaji wa Kituo cha Rusumo, Samweli Mahirane alisema mpaka sasa Wanyarwanda 520 wameshaondoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Ngara na kurejea makwao huku Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fabian Massawe akisema silaha 17 za aina mbalimbali zimesalimishwa.
Mahirane alisema wahamiaji hao wanatokea katika vijiji vya Wilaya za Ngara, Karagwe, Kyerwa, Biharamulo na Geita pamoja na Runzewe na wamekuwa wakiishi katika maeneo hayo bila vibali halali.
“Kuondoka kwa hiari kwa wahamiaji haramu, kutahitimishwa Jumatatu Agosti 12 na baada ya tarehe hiyo, vyombo vya dola vitaanza kufanya kazi kama agizo la Rais Kikwete lilivyoelekeza katika Mikoa ya Kagera na Kigoma,” alisema.
Aliwahakikishia wahamiaji hao usalama katika mataifa yao kwani hivi karibuni Serikali ya Rwanda ilikubali kuwapokea hata walio na mifugo kwa masharti kuwa ndani ya kipindi kifupi wataipunguza kwa kuiuza na kuboresha maisha yao.
“Rwanda wanahitaji mifugo michache, hivyo walio na mingi wanatakiwa kuipunguza kwa kuuza na kujenga makazi bora ikiwa ni pamoja na kuhifadhi ama kulinda mazingira ya nchi hiyo,” alisema Mahirane.

Thursday 8 August 2013

MFANYABIASHARA WA TANZANITE AUAWA KINYAMA...Erasto Msuya

 
 
 
 
 
 
MFANYABIASHARA WA
 TANZANITE AUAWA KINYAMA
Add caption

Habari zilizotufikia hivi punde Kutoka chumba chetu cha habari zinaeleza kuwa mmoja wa Wafanyabiasha wakubwa wa Madini jijini Arusha aliyejulikana kwa jina la

Erasto Msuya, aliyekuwa mmoja wa wafanyabiashara wakubwa wa madini ikiwemo TANZANITE na mmiliki wa SG HOTEL (Pichani) iliyoko Arusha, amepigwa risasi zaidi ya sita na watu wasiojulikana na kufa papo hapo. Polisi walipofika eneo la tukio walikuta mwili wa marehemu ukiwa hatua chache kutoka kwenye gari lake aina ya Range Rover.

Marehemu Erasto alikuwa akitokea KIA kwenda BOMA ambako alikuwa ameitwa na watu (ambao hawakujulikana mara moja) ili wakafanye biashara.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amen.

Wednesday 7 August 2013

Joseph Kony’s LRA

US Congress members sign 

anti-LRA letter to Obama


At least 95 members of the U.S. Congress have signed a letter to President Obama, urging him to sustain U.S efforts in supporting the anti-LRA military operation in central Africa.
Joseph Kony’s LRA has waged war in Uganda and the region for over two decades
This comes after the US Congress was considering a reduction in U.S efforts to address the LRA crisis due to financial constraints and the coup d’état in Central African Republic (CAR).
Joseph Kony's LRA has waged war in Uganda and the region for over two decades Kony and his commanders are wanted by the ICC for war crimes and crimes against humanity. Early this year, President Obama assented to an amended US law which places a cash reward for whoever arrests Kony and his top commanders.
“We believe it is important that the United States remain committed to working with regional forces to protect civilians until the LRA is defeated once and for all,” the letter to President Obama reads in part.
According to a statement released by an international NGO, Invisible Children, the letter will be delivered to President Obama this week, and is sponsored by US Representatives Jim McGovern and Ed Royce, and Senators Jim Inhofe and Mary Landrieu.
Last week, the international NGO Invisible Children petitioned the East African Legislative Assembly (EALA) to intervene and stem the continued security threat posed by LRA to regional stability.
Invisible Children has also launched a campaign urging American activists to ask their legislators to sign the letter to President Obama, with a target of 100 signatures.

Under the campaign dubbed ZeroLRA, Invisible Children is seeking sustenance of support by the US government to the anti-LRA operations until the indicted LRA commanders are apprehended and no child is abducted.
The LRA was kicked out from Uganda by the UPDF five years ago. However, the LRA remains active in South Sudan, Central African Republic (CAR) and DR Congo.
Uganda leads an AU mandated regional taskforce comprising of the LRA affected countries to hunt for Kony and his commanders. In 2011, 100 U.S Special Forces were deployed to advise the regional taskforce.
However, following a coup d’état by Seleka rebels in CAR, the Regional Taskforce deployed against remnants of LRA in South Sudan and Central African Republic (CAR) has not carried out operations against the LRA.

PONDA NI MCHOCHEZI?????

 
 
 
 
 SHEIKH 
PONDA NI MCHOCHEZI?????



MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, amesema Katibu Mkuu wa Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda ni mchochezi sugu mwenye nia ya kumwaga sumu ili kuvuruga misingi ya amani na utulivu nchini.

Balozi Seif alitoa kauli hiyo juzi baada ya kupata futari iliyoandaliwa na Jumuiya ya UVCCM katika ukumbi wa Gymkhana, kisiwani Unguja.

Alisema dhifa za mashirikiano na udugu hufanyika kwenye nchi zilizojengeka amani na si mara zote kufanyika nchi zenye misuguano, vita na mivutano ya kisasa, kijamii na kisiasa.

“Nchi nyingine hukuti haya yakifanyika, huko ni migogoro, mivutano na hasama, hapa tumshukuru Mungu kwa kuwepo na maelewano, umoja na mshikamano wetu,” alisema Balozi Seif.
Akimzungumzia Sheikh Ponda kutokana na hotuba zake, alisema zilikusudia kuigawanya Zanzibar katika vipande vya uchochezi na chuki kwa nia ya kuleta mgawanyiko.

Aidha, Balozi Seif aliwaonya wananchi kutomuunga mkono mtu wa aina hiyo na kuwatahadharisha kuwa kama yangetokea machafuko Sheikh Ponda asingepoteza ndugu wala jamaa visiwani Zanzibar.
“Ponda hana jamaa wala ndugu hapa, si Pemba wala Unguja, uchochezi wake ungeleta vifo na maafa, angesimama kando na kuwacheka Wazanzibari, huyu ni mkaanga mbuyu,” alisema Balozi Seif.

Aliwataka watu kuacha kuonyesha CD za mihadhara yake na kwamba kufanya hivyo kunaweza kuendeleza kupanda chuki na mgawanyiko miongoni mwa Wazanzibari na wenzao wa Bara.

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema Zanzibar haina upungufu wa wasomi wa elimu ya dini za Kikristu na Kiislamu, hivyo kitendo cha kuja Ponda na kuhamasisha chuki hakikubaliki na kutakiwa kulaaniwa.
BALOZI SEIF ASEMA SHEIKH PONDA NI MCHOCHEZI

MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, amesema Katibu Mkuu wa Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda ni mchochezi sugu mwenye nia ya kumwaga sumu ili kuvuruga misingi ya amani na utulivu nchini.

Balozi Seif alitoa kauli hiyo juzi baada ya kupata futari iliyoandaliwa na Jumuiya ya UVCCM katika ukumbi wa Gymkhana, kisiwani Unguja.

Alisema dhifa za mashirikiano na udugu hufanyika kwenye nchi zilizojengeka amani na si mara zote kufanyika nchi zenye misuguano, vita na mivutano ya kisasa, kijamii na kisiasa.

“Nchi nyingine hukuti haya yakifanyika, huko ni migogoro, mivutano na hasama, hapa tumshukuru Mungu kwa kuwepo na maelewano, umoja na mshikamano wetu,” alisema Balozi Seif.
Akimzungumzia Sheikh Ponda kutokana na hotuba zake, alisema zilikusudia kuigawanya Zanzibar katika vipande vya uchochezi na chuki kwa nia ya kuleta mgawanyiko.

Aidha, Balozi Seif aliwaonya wananchi kutomuunga mkono mtu wa aina hiyo na kuwatahadharisha kuwa kama yangetokea machafuko Sheikh Ponda asingepoteza ndugu wala jamaa visiwani Zanzibar.
“Ponda hana jamaa wala ndugu hapa, si Pemba wala Unguja, uchochezi wake ungeleta vifo na maafa, angesimama kando na kuwacheka Wazanzibari, huyu ni mkaanga mbuyu,” alisema Balozi Seif.

Aliwataka watu kuacha kuonyesha CD za mihadhara yake na kwamba kufanya hivyo kunaweza kuendeleza kupanda chuki na mgawanyiko miongoni mwa Wazanzibari na wenzao wa Bara.

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema Zanzibar haina upungufu wa wasomi wa elimu ya dini za Kikristu na Kiislamu, hivyo kitendo cha kuja Ponda na kuhamasisha chuki hakikubaliki na kutakiwa kulaaniwa.

Vuai alisema Zanzibar ina hazina kubwa ya wasomi wenye upeo na ujuzi mkubwa wa masuala ya dini, kwani masheikh wake ndio waliofanya kazi kubwa ya kuzifikisha dini zote hadi Kigoma.
PONDA NI MCHOCHEZI?????

Vuai alisema Zanzibar ina hazina kubwa ya wasomi wenye upeo na ujuzi mkubwa wa masuala ya dini, kwani masheikh wake ndio waliofanya kazi kubwa ya kuzifikisha dini zote hadi Kigoma.

Tuesday 6 August 2013

Matukio ya Afrika

Matukio ya Afrika

Uhamiaji Group

Matukio ya Afrika

Somalia: Puntland lasitisha uhusiano wake na serikali

Eneo lenye utawala wake nchini Somalia, Puntland limesema limesitisha uhusiano wake na serikali kuu ya taifa hilo kwa kuituhumu kukataa pendekezo la kugawana madaraka na serikali kuu ya Somalia.
Kutoka Mogadishu Sudi Mnette amezungumza na Mbunge, Hussein Bantu na kwanza alitaka kujua hatua hiyo wameipokeaje? Kusikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.