Saturday 27 July 2013

 
 
 
 
WALIOKUWA WANATAKA MUUNGANO WA
 MKATABA WAANZA KUBABAIKA
WALIOKUWA WANATAKA MUUNGANO WA MKATABA WAANZA KUBABAIKA

Tume ya Mabadiliko ya KAtiba imeendelea kupokea maoni ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba huku hoja ya kuwepo kwa muungano wa mkataba ikionekana kutokuungwa mkono na wajumbe wengi.

Wakitoa mawazo yao kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Ecrotanal Kisiwani Unguja chini ya Kamishna wa Tume Awadh Said Ali, wajumbe wa mabaraza ya Katiba ya Wilaya walieleza kuwa wanaodai Serikali tatu, Muungano wa mkataba au kuvunja muungano wana jazba ambazo ni hatari kwa uhai wa visiwa vya Zanzibar. 

Mjumbe Khalid Salehe Mwina alisema “Muundo wa Serikali mbili ubakei, haiwezekani mgonjwa aumwe mguu apasuliwe kichwa. Zanzibar eneo letu la ardhi, ambayo ndio kimbilio la watu maskini kama sisi, ni dogo tofauti na bara, tusijitenge na kushindwa kutumia fursa za kiuchumi zilizoko bara.”    

Idadi kubwa ya wajumbe walisema Serikali mbili hazina matatizo kwa wananzi labda kwa viongozi waroho wa madaraka. Isipokuwa walisisitiza kuwa kero za Muungano zinapaswa kushughulikiwa kwa wakati. Hoja za wengi zilijikita katika uwezo ulioonyeshwa na Serikali mbili katika kulinda amani, utulivu na umoja wa kitaifa.

(Kwa habari mbalimbali tembelea : http://www.dar24.com)

Tume ya Mabadiliko ya KAtiba imeendelea kupokea maoni ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba huku hoja ya kuwepo kwa muungano wa mkataba ikionekana kutokuungwa mkono na wajumbe wengi.

Wakitoa mawazo yao kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Ecrotanal Kisiwani Unguja chini ya Kamishna wa Tume Awadh Said Ali, wajumbe wa mabaraza ya Katiba ya Wilaya walieleza kuwa wanaodai Serikali tatu, Muungano wa mkataba au kuvunja muungano wana jazba ambazo ni hatari kwa uhai wa visiwa vya Zanzibar.

Mjumbe Khalid Salehe Mwina alisema “Muundo wa Serikali mbili ubakei, haiwezekani mgonjwa aumwe mguu apasuliwe kichwa. Zanzibar eneo letu la ardhi, ambayo ndio kimbilio la watu maskini kama sisi, ni dogo tofauti na bara, tusijitenge na kushindwa kutumia fursa za kiuchumi zilizoko bara.”

Idadi kubwa ya wajumbe walisema Serikali mbili hazina matatizo kwa wananzi labda kwa viongozi waroho wa madaraka. Isipokuwa walisisitiza kuwa kero za Muungano zinapaswa kushughulikiwa kwa wakati. Hoja za wengi zilijikita katika uwezo ulioonyeshwa na Serikali mbili katika kulinda amani, utulivu na umoja wa kitaifa.

(Kwa habari mbalimbali tembelea : http://www.dar24.com/)

No comments:

Post a Comment