Saturday 20 July 2013

Polisi Mwanza


Majambazi wavamia kituo
kikuu cha Polisi Mwanza



Wizi huo wa ajabu ulitokea Julai 18, mwaka huu, ambapo majambazi hao walivunja kituo hicho ambacho ndani yake kuna Ofisi ya Mkuu wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC).


Mwanza. Majambazi wamevunja ofisi za Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Mwanza na kuiba mali mbalimbali vikiwemo vielelezo vya watuhumiwa walio na kesi mahakamani.
Wizi huo wa ajabu ulitokea Julai 18, mwaka huu, ambapo majambazi hao walivunja kituo hicho ambacho ndani yake kuna Ofisi ya Mkuu wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC).
I.G.P..MWEMA
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zilibaini kuwa majambazi hao walivunja ghala la vielelezo vya washtakiwa, chumba cha ghala la vipuri vya magari ya polisi, zikiwemo ofisi za Wapelelezi wa Makosa ya Jinai na Waendesha Mashtaka.
Majambazi hao wanadaiwa kuiba majalada ya kesi, begi lililokuwa na vielelezo vya washtakiwa, kompyuta ndogo mbili (Laptop) za ushahidi na kutoweka.
Wizi huo uliotokea usiku na kubainika asubuhi, ambapo watu hao ambao idadi yao haijajulikana wanadaiwa waliweza kufanikiwa kuingia ndani ya ofisi hizo za polisi, kwa kuvunja madirisha mawili ya chumba cha ghala la ofisi za Mkaguzi wa Elimu Kanda ya Ziwa ambazo zinapakana na Kituo Kikuu cha Polisi cha Kati cha Jijini Mwanza, kisha kufanikisha wizi huo.
Habari zilizopatikana kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zinaeleza kwamba wizo huo ambao ulilenga ofisi ya vielelezo na mashtaka, ulipangwa kwa umakini na kutekelezwa bila ya polisi waliokuwa zamu usiku huo kubaini lolote.
Kwa mujibu wa maelezo wezi hao inadhaniwa ni watu wenye uzoefu na jengo hilo, wakiwa na nia ya kuchukua vielelezo mbalimbali pamoja na mafaili muhimu ya kesi kubwa.
Hili ni tukio lingine kubwa kutokea kwa Jeshi la polisi Mkoa wa Mwanza sambamba na tukio la kuuawa kwa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, Oktoba 13, mwaka jana ambaye alipigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi saa nane usiku wakati akitoka katika kikao cha harusi.
Kauli ya Kamanda Mangu:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Evarist Mangu, amethibitisha kutokea kwa wizi huo na kusema jeshi lake linafanya uchunguzi wa kina kubaini waliohusika, na kusisitiza kuwa kama ni askari wake ama watu toka nje hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Alisema wezi hao waliingilia katika ofisi ya Ukaguzi Elimu Kanda ya Ziwa ambako walivunja madirisha mawili, moja likiwa ni kuingia ndani ya ghala la ofisi za elimu na dirisha lingine la kutokea nje ya ghala hilo, kisha kuvunja dirisha la ndani ya majengo ya polisi na kufanikisha wizi huo.
“Wezi hao walipiga jeki nondo za madirisha hayo, hivyo kung’oka na kuingia ndani kisha kwetu, walianza kuingia katika ghala la polisi la kuhifadhia vifaa vya ofisi vya Jeshi la polisi, lakini inaonekana walikosa cha kuiba, huko walipanda darini na kutokea katika chumba kingine nako hawakuiba, lakini katika chumba cha vielelezo ambako walikuta begi lililokuwa na nguo za vielelezo pamoja na kompyuta ndogo mbili, Lap Top, ambazo walitoweka nazo,” alieleza Kamanda Mangu.
Chumba kingine kinachodaiwa kuvunjwa katika wizi huo ni chumba kinachotunza vipuri vya magari vilivyotumika, ambako Kamanda alidai kuwa hakuna kilichoibwa pamoja na chumba cha vielelezo walikochukua begi la vielelezo.
Mkaguzi wa Elimu Kanda:
Kwa upande wake kaimu Mkaguzi wa Elimu Kanda ya Ziwa, Florencia Vicent, alisema wao hawakugundua wizi huo kutokana na chumba kilichovunjwa kuwa ni ghala, ambacho hakifunguliwi kila mara na kwamba hakikuwa na vitu zaidi ya milango mibovu na maboksi tupu.
“Asubuhi mkaguzi mwenzangu alinieleza kamba wamefika polisi hapa na kudai tumeibiwa hivyo tuliamua kufungua stoo yetu na kuangalia, ambapo tulibaini kuvunjwa kwa madirisha hayo mawili pamoja na dari, lakini inaonekana kama walikuwa wakitafuta njia ya kuingilia na kutoka polisi baada ya wizi,” alieleza mkaguzi huyo.
Alisema ndani ya ghala lao waliweza kukuta suruali mbili mpya moja ikiwa ni aina ya jinsi na nyingine kadeti vikiwa vimetelekezwa ambapo polisi walivitambua kama ni sehemu ya vielelezo vyao na kuondoka navyo.
“Hapa tunaye mlinzi lakini, analinda eneo la ofisi zetu, eneo ambako wezi wameingia lipo chini ya polisi na lina mlango ambao hutumika kupitishia mahabusu, huko wapo polisi, hivyo inaonekana kwetu hakuna kitu kilichoibiwa, mpaka sasa tumefanya ukaguzi wa kina lakini hatuna kitu ambacho kimeibiwa, walengwa katika wizi huo ni polisi na hapa ilikuwa kama njia,” alifafanua kaim

No comments:

Post a Comment