Wednesday 4 September 2013

Tanapa yawataka wananchi kulima mazao mbadala



Swala

Twiga

Simba
Pangani. Hifadhi ya Taifa Tanapa, imewataka wananchi waishio karibu na
hifadhi za wanyamapori nchini, kubadilika na kuacha tabia ya kuishi kimazoea badala yake wawe wabunifu kwa kupanda mazao ambayo hayashambuliwi na wanyama waishio katika maeneo ya mbuga za wanyama.
Meneja Ujirani Mwema Taifa, Ahmed Mbugi alisema endapo wakazi wa maeneo jirani watapanda mazao kama ufuta, pilipili za kuwasha pamoja na miti ya kutanda itasaidia kuzuia njia za wanyama kupita kwenye maeneo yao.
Hayo aliyasema wakati wa mafunzo ya uandishi wa masuala ya hifadhi yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Vijijini na Mazingira na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wilayani Pangani hivi karibuni.

Tanga Kwetu

No comments:

Post a Comment